5G yaanza kupatikana katika nchi ya kwanza Afrika. Baada ya ‘figisu figisu’ za mataifa ya Marekani na baadhi ya washirika wake wa ‘kuibania’ kampuni ya Huawei juu ya usambazaji wa teknolojia yake ya kisasa zaidi ya mtandao wa 5G, kampuni hiyo imepeleka teknoljia hiyo nchi ya Afrika Kusini.

Huawei kwa kushirikiana na kampuni inayotoa huduma za mawasiliano ya nchini Afrika Kusini ya RAIN, wamefanikiwa kuwezesha teknolojia ya mtandao wa 5G nchini humo.
Hatua hiyo inaifanya nchi ya Afrika Kusini kuwa nchi ya kwanza ya Bara la Afrika kuwa na teknolojia ya mtandao wa 5G ambao una kasi zaidi ya mara 10 ya mtandao wa 4G.
Awamu ya kwanza ya usambazaji wa teknolojia hiyo itahusisha miji miwili kabla ya kusambazwa nchi nzima.
Maeneo muhimu ya miji ya Johannesburg na Pretoria ndio itanufaika na awamu ya kwanza ya usambazaji wa 5G.
Mtandao huo wa 5G unatarajiwa kuwa na kasi ya MB 200 kwa sekunde mpaka MB 700 kwa sekunde.