Leo nitakufundisha jinsi gani ya kulazimisha moja kwa moja simu yako kupokea signo za mfumo wa aina flani tuu, – yaani 2G (GSM), 3G (WCDMA), 4G au vyovyote vile utakavyopendelea.
Kwa siku kadhaa nimekuwa nikitumia mtandao wa Smart ambao tumefanikiwa kuingia nao mkataba wa kutudhamini kwa huduma za intaneti na mawasiliano.
Changamoto ilikuja pale ambapo kwenye baadhi ya maeneo kutokana na sababu mbalimbali simu yangu inaondoa mfumo wa 4G na kwenda kwenye 3G bila ulazima. Inafanya hivyo kama signo za 4G zikiwa chini ingawa zikiwa zinatosha kabisa kwa kuendelea kunipa kiwango kizuri cha spidi ya kudownload ukilinganisha na mfumo wa 3G. Jambo ili likanifanya nichunguze kama kuna njia rahisi ya kulazimisha simu ipokee signo za 4G tuu.
Kama nipo busy na kitu mfano kuangalia video za YouTube hili linakuwa tatizo, so nikaanza kuchambua kuhusu kulazimisha simu yangu ichukue signo za 4G tuu.
‘Simu kuhama hama signo za mtandao hutumia kiwango kikubwa cha chaji ya simu yako katika kuhama hama ukilinganisha na kama simu hiyo ikiwa inapokea signo ya aina moja tuu’
Kuna baadhi ya simu zinasehemu rahisi za kulazimisha hili katika eneo la settings (yaani mipangilio) lakini zingine zinakupa chaguo la kupendelea (prefer) 3G kama ipo na kama simu ikiona signo chache basi inakurudisha kwenye 2G. Leo nitakufundisha jinsi gani ya kulazimisha moja kwa moja simu yako kupokea signo za aina flani tuu, – yaani 2G (GSM), 3G (WCDMA), 4G au vyovyote vile utakavyopendelea.
Hatua
> Kwenye sehemu ya kupiga simu (Dialer), andika na piga *#*#4636#*#* (hakikisha ni sahihi kama ilivyo), kisha piga.
> Itakuja chaguo – Ingia ‘Phone Information’,
> Kisha ingia ‘Preferred network type’
Kulingana na simu yako basi utaweza kuona machaguo mbalimbali.
Kwenye simu nyingi utaona GSM, WCDMA, na WCDMA preffered, kwa simu zenye uwezo wa LTE (4G) utaona pia LTE.
1. WCDMA prefferred – mpangilio huu utakuwa unapendelea signo za 3G ila kama hazipo basi simu itapokea signo za 2G
2. WCDMA only – mpangilio ni kulizamisha simu kupokea signo za 3G tuu na hivyo kama hazipo utakosa signo kabisa kwenye simu
3. GSM only – mpangilio huu utaweka simu kwenye mfumo wa 2G tuu. Mfumo huu ni mzuri kama hutumii huduma za intaneti sana/kabisa, kwani unatumia chaji ya simu kidogo sana
4. LTE/CDMA auto – mpangilio huu utafanya simu yako kuhama kati ya mfumo wa 3G na 4G kulingana na upatikanaji wa signo
> Chagua kulingana na upendavyo, mabadiliko yatatokea mara moja na kama hayajatokea basi zima na kuwasha simu na hilo litakuwa limefanyika.
Soma Pia – Fahamu Tofauti Kuu Kati ya Teknolojia za 2G, 3G, 4G n.k
Uwezo huu unapatikana zaidi kwenye simu nyingi za Android za kuanzia toleo la Android 4.4 na kuendelea. Ni simu chache tuu ndio watengenezaji wamezuia uwezo huo, jaribu na utuambie kama kwako umefanikiwa. Endelea kutembelea mtandao wa TeknoKona
Simu yangu haiaccess whatsapp,, nikitumia Wi-Fi inakubali ila nikiweka mb za kawaida inakataa, inaniletea neno YOU MAY HAVE MESSAGES ON YOUR WHATSAPP.
Nilijaribu ku-uninstall na kuinstall tena lakini haiwezekani.. Je nifanyeje ili ikubali. Tatizo lilianza baada ya kurestore simu. Natumia TECNO W3LTE
Natumia Samsung Galaxy J2, nmetumia *#*#4636*#*# nimefuata hatua zote kama mlivoelekeza ili kulazimisha mtandao wa 3G, lakini inaniambia namba nayopiga siyo sahihi
Nenda Uka I flash Ina Wezeka Wakat Una Restore Il Kua Na Chaji Ndo Ndio Huwa Zina Leta Matatizo Kama Hayo
ya kwang ni k7 lkn haikubal kupanda 3G na nieka 3G inajiandika Emargency only nifanyaj
Nimejaribu kuset lakini simu yangu Pop2 power inapandisha 3G kwa uchache sana zaidi ni kupoteza signal na kuandika emmegency call only,,,Nifanyeje wakuu huku kwetu IT hakuna kabisa
Itakuwa signal za 3G zipo kwa uchache sana eneo hilo upo
Natumia itel 1503 nimeijaribu imegoma je simu yangu sio ya android?