AI Yamfufua Val Kilmer. Takribani mwaka mmoja tangu kifo cha mwigizaji nguli wa Hollywood, Val Kilmer (aliyeaga dunia Aprili 2025), ulimwengu wa teknolojia na filamu umetikiswa na habari mpya. Kupitia nguvu ya Akili Mnemba (Generative AI), Kilmer anatarajiwa “kurejea” kwenye uigizaji katika filamu mpya ya “As Deep as the Grave”.
Hii si mara ya kwanza AI kutumika, lakini ni mara ya kwanza kwa mwigizaji aliyefariki kupewa uhusika mkubwa (lead role) kwa kutumia teknolojia inayochanganya sauti na sura yake kikamilifu bila yeye kuwahi kufika eneo la kurekodia (set).

Kilichotokea: Kutoka “Top Gun” hadi AI
Val Kilmer alipoteza sauti yake kutokana na saratani ya koo miaka ya nyuma, jambo lililopelekea atumie teknolojia ya Sonantic (ambayo nayo ni ya AI) kurudisha sauti yake alipotokea kwenye filamu ya Top Gun: Maverick (2022). Mpango wa muvi hii mpya, ulianza kufumwa tokea miaka mitano nyuma kupitia urafiki wa karibu wa mtayarishaji wa muvi Coerte Voorhees na muigizaji Val Kilmer. Hata hivyo, baada ya kifo chake mwaka jana, muongozaji Coerte Voorhees aliamua kutotumia mwigizaji mwingine, kwani stori nzima aliifuma kwa haiba ya Val Kilmer, hivyo kwa ukuaji wa teknolojia ya AI kwa sasa, ameona ni bora kuitumia kukamilisha uhusika wa Kilmer kama “Father Fintan”.

Teknolojia Inayotumika
Tofauti na teknolojia za zamani za CGI, filamu hii inatumia mifumo ya kisasa ya Generative AI:
- Visual Reconstruction: Walitumia picha za zamani za Kilmer na video za miaka yake ya mwisho kutengeneza “digital double” – kopi ya kidigitali, inayoweza kuendeshwa na kutumika katika kuonesha hisia na kufanya matendo mbalimbali.
- Voice Synthesis: Sauti yake imetengenezwa upya kwa kutumia rekodi zake za zamani, ikitoa mtindo wa sauti ile ile iliyomfanya kuwa maarufu duniani.
Movies ya As Deep as the Grave ipo kwenye hatua za mwisho inasubiria kupewa tarehe ya kuingia Sinema.
Maadili na Mashaka:
Je, Hii ni Sawa? Hatua hii imezua mjadala mzito kuhusu maadili ya kidijitali. Hata hivyo, familia ya Kilmer (akiwemo binti yake Mercedes) imetoa baraka zote kwa mradi huu, ikisema kuwa Val alikuwa mpenzi mkubwa wa teknolojia mpya na angependa kuona sanaa yake ikiendelea hata baada ya kifo chake.
Kwa wasomaji wa Teknolojia.co.tz, hili ni funzo kuwa sasa tuko kwenye enzi ambapo kifo si kikwazo tena cha kuonekana kwenye filamu. Hii inafungua mlango kwa “digital legacy” ambapo mwigizaji anaweza kuendelea kufanya kazi hata karne moja baada ya kuondoka duniani huku kizazi chake kikiendelea kunufaika na malipo ya ushiriki huo.
No Comment! Be the first one.