Akiliunde, AI (Artificial Intelligence) ni teknolojia mpya inayokua kwa kasi kubwa kwa sasa. Katika moja ya maeneo ambayo wadau wengi wamekuwa wakiwa na maoni tofauti ni kwenye athari za teknolojia hii katika sekta ya ajira.
Sasa ni rasmi wadau wengi wanakubaliana teknolojia hiyo haitaathiri tu ajira miaka michache baadae bali imeshaanza kuathiri sekta hiyo kutokana na wafanyakazi wengi kujikuta wakipoteza ajira na wale wanaobaki kwenye ajira inawabidi wajifunze utumiaji wa AI ili kuboresha ufanisi katika kazi zao.
Kuna makisio ya watu takribani milioni 300 kupoteza ajira zao kutokana na ukuaji wa matumizi ya AI katika kipindi cha mwaka mmoja (Chanzo Goldman Sachs). Mkurugenzi wa kampuni ya utengenezaji magari ya FORD amesema anatarajia nusu ya wafanyakazi wao wa ofisini kupoteza ajira zao kutokana na utumiwaji wa teknolojia ya AI katika kuboresha ufanisi wa kazi katika kampuni hiyo.
Katika sekta za kwanza kabisa kuathirika ni sekta ya teknolojia, sekta iliyoibuni na kuleta teknolojia ya akiliunde. Kwa mwaka 2024 pekee watu zaidi ya 150,000 walipoteza ajira zao katika sekta ya teknolojia kutokana na kuongezeka kwa utumiaji wa AI.
Athari kwa Kazi za Ofisini
Upotevu wa ajira unagusa sekta nyingi zaidi ya teknolojia. Kazi zinazotegemea majukumu ya kawaida yanayoendeshwa na data ndizo zilizohatarini zaidi kuliko sekta zingine.
Kiwango cha Hatari ya ajira kuathirika kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya AI.

Google imepunguza wafanyakazi 500 mwezi Mei kutokana na maboresho ya ufanisi kutokana na utumiaji wa mifumo ya AI. Microsoft wanategemea kupunguza asilimia 5 ya wafanyakazi wao wote mwaka huu.
Ni nini kifanyike?
Mkakati wa wafanyakazi kujiongeza kiujuzi – sio elimu, ndiyo suluhisho kubwa pendekezwa. Na watafiti wengi wanaona ni jukumu la kila mfanyakazi kujitathimini na kufanya maamuzi ya kuongeza ujuzi kabla ya athari hizi za ukuaji wa matumizi ya AI kumfikia.
No Comment! Be the first one.