Kama ulikuwa unasubiri kununua kompyuta mpya ya Mac au iPad, huenda ukatakiwa kutoa pesa nyingi zaidi. Mapema leo, Apple imesasisha katika duka lake la mtandaoni na kuweka bei mpya zinazoonesha ongezeko kubwa la kati ya dola $100 hadi zaidi ya $300 kwenye bidhaa zake kadhaa maarufu – ongezeko la takribani Tsh 500,000 hadi Tsh 800,000 si la kawaida.

Hatua hii inakuja wiki moja tu baada ya Mtendaji Mkuu (CEO) wa kampuni hiyo, Tim Cook, kuonya kuwa kupanda kwa gharama ya vipuri vya kumbukumbu (RAM na storage chips) kungemfanya achukue maamuzi magumu.
Bei Mpya Zikoje?
Mabadiliko haya yameathiri takribani matoleo yote ya Mac na iPad, huku bei za simu za iPhone zikibaki vilevile kwa sasa. Tazama mabadiliko ya bei za kuanzia (Base Models):
| Kifaa | Bei ya Zamani | Bei Mpya | Ongezeko |
| MacBook Neo | $599 | $699 | +$100 |
| MacBook Air (512GB) | $1,099 | $1,299 | +$200 |
| MacBook Pro (1TB) | $1,699 | $1,999 | +$300 |
| iPad Air (128GB) | $599 | $749 | +$150 |
| iPad Pro | $999 | $1,199 | +$200 |

Nini Kinasababisha Hali Hii?
Sio siri kuwa soko la teknolojia kwa sasa linatawaliwa na Mapinduzi ya Akili Mnemba (AI). Makampuni makubwa yanayojenga vituo vya data (Data Centers) vya AI yamekuwa yakinunua kwa wingi chipu za kumbukumbu (DRAM na NAND) kutoka kwa wazalishaji kama Micron.
RAM na diski za storage/uhifadhi zinategemea vipuri hivi muhimu ambayo vinahitajika kwa wingi kwa sasa kwa ajili ya vifaa vya sekta ya soko la AI.
Uhitaji huu mkubwa umesababisha bei za chipu hizo kupanda mara nne ndani ya miezi 12 iliyopita. Wazalishaji wengi wa kompyuta kama Dell, HP, na Lenovo walishapandisha bei zao mapema, na sasa Apple—ambayo ilikuwa ikijitahidi kuwakinga wateja wake—imeshindwa kuhimili vishindo.
Katika taarifa rasmi, msemaji wa Apple alisema:
“Hatujawahi kuona bei ya kipuri ikipanda kwa kiasi kikubwa na kwa haraka hivi… Tumefikia hatua ambapo tunalazimika kuanza kupandisha bei kwenye bidhaa kadhaa.”
Mtazamo wetu
Apple inajulikana kwa kuwa na ushawishi mkubwa kwenye minyororo ya usambazaji, lakini hatua hii inaonesha kuwa hakuna kampuni iliyo salama dhidi ya “Tsunami ya AI.” Ikiwa hata kompyuta yao ya bei nafuu zaidi, MacBook Neo, imepanda kwa $100 (takribani laki 2.7 hadi 3), ni wazi kuwa gharama za uzalishaji zimekuwa kubwa mno.
No Comment! Be the first one.