Bodi ya uchambuzi wa filamu Kenya (KFCB) imesema kwamba ni lazima huduma ya NETFLIX ifuate sheria za filamu za Kenya na kama watakiuka sheria hizo basi watafungiwa kurusha huduma zao.
KFCB inasema kwamba imegundua kwamba NETFLIX ina filamu na tamthilia ambazo hazifuati sheria zilizowekwa kutawala sekta ya filamu, KFCB imesema inategemea kukutana na NETFLIX siku ya Jumatatu na kisha kujadili sera za Kenya katika filamu za nje.
Afisa mtendaji mkuu wa KFCB Ezekiel Mutua amesema kwamba watatumia sheria ya filamu na Maigizo ambayo inashughurika na kusimamia filamu, pia aliongeza sheria ya mawasiliano na habari inawapa mamlaka ya kufungia ama kuweka vikwazo filamu zinazorushwa na vituo kwa mtandao ama kwa njia ya kawaida.
Katika kauli yake kwa gazeti la Business Daily Mutua amesema kwamba wangeweza kuwafungia NETFLIX kwa kuleta bidhaa bila ya wao KFCB kuzichambua, hata hivyo amesema kwa kuwa hawataki kuwaogopesha wawekezaji wa kigeni basi wataenda na kuwaona NETFLIX na kuwaambia viwango vya filamu za Kenya.
NETFLIX imekuwa ni gumzo katika viunga vya Nairobi tangu ilipotangazwa kuwa huduma hii itaanza pia kupatikana Kenya, kwa vyovyote vile italeta taflani endapo kwa namna yeyote ile KFCB itaifungia huduma hii. Ukweli ni kwamba kisheria KFCB wanayo haki ya kufungia huduma ya NETFLIX ila je ni kweli kwamba kila filamu inayorushwa inakidhi vigezo vya bodi hii?
Kipindi cha nyuma KFCB ilishwa wahi kufungia baadhi ya filamu kuoneshwa,kuuzwa ama kusambazwa ndani ya Kenya kutokana na kukiuka vigezo, baadhi ya filamu zilizowahi kufungiwa ni pamoja na “The Wolf of Wallstreet na The shades of Grey.
No Comment! Be the first one.