Utumiaji wa intaneti watawaliwa na bots. Kile kilichokuwa kikitabiriwa kutokea miaka michache ijayo kimefika mapema. Kwa mara ya kwanza katika historia, idadi ya maombi ya kurasa za wavuti (HTTP requests) yanayofanywa na programu za kompyuta (bots) imepita yale yanayofanywa na binadamu.
Takwimu mpya kutoka kwa kampuni kubwa ya ulinzi wa mifumo ya wingu, Cloudflare, zinasema kuwa mifumo ya kiotomatiki sasa inazalisha takriban 57.5% ya trafiki yote ya internet duniani, huku binadamu wakibakiwa na 42.5% tu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Cloudflare, Matthew Prince, amekiri kushangazwa na kasi hii:
“Nilidhani hili lingetokea mwaka 2027. Lakini trafiki ya mifumo ya AI (agentic traffic) inakua kwa kasi kubwa sana kiasi kwamba bots sasa wameipita trafiki ya binadamu mtandaoni.”
Mapinduzi ya “AI Agents”
Tofauti na zamani ambapo bot nyingi zilikuwa ni za udukuzi au mifumo ya utafutaji (kama Googlebot), ongezeko la sasa linachochewa na Agentic AI—wasaidizi wa kidijitali wa AI wanaotafuta data, kulinganisha bei, au kukusanya maudhui kwa niaba ya binadamu. Roboti mmoja wa AI anaweza kufungua maelfu ya kurasa ndani ya sekunde chache, jambo linalozalisha trafiki kubwa ya ghafla.
Binadamu bado tunaongoza kwa muda tunaotumia mtandaoni (engagement) kama kuangalia video za YouTube na TikTok, lakini shughuli hizo hazizalishi idadi kubwa ya “HTTP requests” za haraka kama wanavyofanya bots.
Changamoto kwa Wamiliki wa Tovuti
Hali hii inaleta changamoto mbili kuu:
- Gharama za Seva: Bots wanatumia bandwidth kubwa, jambo linaloweza kuzifanya tovuti kuwa nzito au kuanguka.
- Kupotea kwa Mapato: AI inaposoma maudhui na kumpelekea mtumiaji jibu la moja kwa moja, tovuti husika inapoteza wageni (traffic) na mapato ya matangazo.

No Comment! Be the first one.