Messenger app ya Facebook kwa ajiri ya kuchati ipo mbioni kuleta njia tatu mpya kwaajiri ya kuweza ku-add marafiki katika app hiyo, huu ni ushahidi kwamba Messenger inajaribu kupambana na Snapchat na mitandao mingine kupata watumiaji wapya.
Mtandao huu unajaribu kuwa mtandao rafiki kwa watumiaji kwa maana jinsi mtandao unavyokuwa ni rahisi kutumia ndivyo ambavyo mtandao unavyoweza kupata wateja wengi na kuwa maarufu.

Messenger imeleta namna zifuatazo mpya za kuweza ku-add marafiki katika mtandao huu kama ifuatavyo
-
Kuadd marafiki kwa kutumia username.
Hii ni njia ambapo mtumiaji anaweza kumuongeza rafiki katika orodha ya marafiki wake kwa kuandika jina ambalo mtumiaji analitumia katika Messenger. Njia hii sio ngeni kwani ndiyo inatumiwa na mitandao mingine ya kijamii kama vile Twitter.
-
Ku-add marafiki kwa kutumia link.
Njia hii itawapatia watumiaji link ambayo unaweza kuwapatia marafiki zako kwa njia yeyote ile na pindi watakapo bofya linki hiyo watapelekwa moja kwa moja katika ukurasa wako wa Messenger.
-
Ku-add marafiki kwa kutumia Code.
Hii ni njia mpya ambayo tumeanza kuiona sana katika mtandao wa Snapchat, njia hii inamtengenezea code mtumiajia ambapo ili kumuadd rafiki yako unatakiwa kui scan code hiyo ambayo itakupeleka moja kwa moja katika ukurasa wa rafiki yako.
Yote kwa yote hizi ni jitihada za Messenger kuweza kubaki katika chati hasa katika kitengo hichi cha mitandao ya kijamii ambacho kwa siku za karibuni kimekuwa na ushindani mkubwa sana.
One Comment
Comments are closed.