Kampuni la Samsung lipo mbioni kuja na simu janja ya Note 6. Simu hii bado haijatoka lakini vyanzo mbali mbali vimeandika kuhusu fununu za ujio huo. Leo teknokona imekuandalia fununu hiyo kwa ufupi
Kampuni la Samsung lina mafanikio makubwa sana na mafanikio hayo kwa kiasi kikubwa yametokana na mauzo ya simu zake
Kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana kwa kampuni kwa kupitia matoleo yao ya ‘Note’ Samsung wameona wasilale na kuendelea kutoa matoleo ya simu hizi ikiwa yana maboresho mengi zaidi kulingana na soko.

Kwa sasa kampuni inategemewa kuja (kutoa) toleo lake la Note 6 kwani kwa sasa Note 5 iko tayari sokoni. Simu hii bado haijatoka na kuna fununu kadha wa kadha juu yake.
Simu hii inategemewa kuwa na ukubwa wa kioo cha inchi 5.8 na itakuwa na GB 6 za ukubwa wa RAM. Licha ya kuwa Note 5 haikufanya vizuri sana mwaka jana (ilipo achiwa) hili bado halijawakatisha tamaa Samsung. Bado wanapambana kuhakikisha bado wanamiliki soko lao kwa kufanya maboresho zaidi.
Lakini kama ukiniuliza mimi kwanini mauzo ya Note 5 yalifanya vibaya ntakuambia sababu ni kwamba walitoa simu mbili kali sana za mwendelezo wa Galaxy S ( S6 na S6 Edge). Hili ni moja kati ya mambo ambayo yalipunguza mauzo ya simu hizo kwani matoleo hayo mawili yalishika soko sana.
Lakini kwa mteja ambaye anapenda simu za Samsung za mfumo ule wa Note humwambii kitu kutokana na simu hizi.

Fununu ni kwamba simu hizo zitatokwa kwa matoleo ya aina tatu; Standard, Edge na nyingine katika mfumo wa kukunja. Fununu hizi zimetoka katika vianzo mbali mbali hivyo zinaweza kuwa ni fununu tuu
Note 6 inasemekana kuwa itakuwa na betri la uwezo wa mAh 4500 na pia itakuwa na wembamba mkubwa tuu. Na vile vile inategemewa kwa kiasi kikiubwa kuja na programu endeshaji (OS) mpya ya Android N.
MUHIMU: Samsung bado wao hawajatoa taarifa kamili kuhusiana na ujio wa simu hii hivyo usije ukashangaa kuwa hakutakuwa na simu kama hiyo kutoka Samsung au ikatoka sema ikawa na sifa tofauti kama hizi tolizoandika.