Google kushirikiana na Fiat Chrysler. Kwa kipindi kirefu Google walishakuwa wazi ya kwamba ingawa wamejikita sana katika utengenezaji wa teknolojia ya magari yajiendeshayo yenyewe mwisho wa siku wao hawatajiingiza kwenye biashara ya utengenezaji wa magari.
Inasemekana Google na Fiat Chrysler Automobiles wapo njiani kukamilisha makubaliano ya utengenezaji wa magari hayo.
Moja ya magari yanayotumiwa na Google yenye mfumo wa kujiendesha yenyewe
Kampuni ya Fiat Chrystler ni kampuni kubwa katika biashara ya magari na hivyo kwa Google kupata m-bia katika utengenezaji wa magari hayo ni dalili nzuri katika hatua ya kuleta magari hayo sokoni.
Katika uhusiano huu; Google atakuwa anachangia mfumo wa teknolojia wakati Fiat Chrysler inachangia ujuzi, kiwanda na uingizaji wa magari hayo sokoni.
Uhusiano huu unaweza fananishwa na uhusiano uliopo kati ya Google na makampuni kama vile HTC, Samsung na wengine katika utengenezaji wa simu spesheli za Google zinazofahamika kwa jina la Nexus…ambapo Google wanasimamia ubunifu wote, utengenezaji unafanywa na makampuni mengine uku suala zima la matangazo (marketing) ya simu hizo ukifanywa na Google.
Kwa sasa kwa miaka mingi Google wamekuwa wakitumia toleo spesheli la gari la Toyota Lexus x450h walilolifanyia maboresho mbalimbali ili kulipa uwezo wa teknolojia hiyo
Suala la maendeleo mazuri ya mazungumzo kuhusu Google kushirikiana na Fiat Chrysler zimevujishwa na mtu anayehusika katika mazungumzo hayo – habari hizo zilitolewa kwa shirika la utangazaji la Reuters. Google na Fiat Chrysler wote hawajatoa taarifa rasmi kuhusu mazungumzo hayo.
Kwa kipindi kirefu inafahamika Google (Tawi la kampuni mama ya ALPHABET) wamekuwa wakijaribu kufanikisha suala hili na makampuni mengine makubwa ya utengenezaji magari kama vile Ford Motos, General Motors n.k lakini makampuni hayo yalikuwa hayajavutiwa na ushirikiano na kampuni ya Google. Matokeo yake kampuni kama vile General Motors wamejiingiza wenyewe pia katika utengenezaji wa teknolojia hiyo kivyao vyao.
Kwa muda wa miaka hii kadhaa teknolojia ya magari yajiendeshayo imekuwa inakua kwa kasi, sasa hivi si Google tuu waliojikita katika teknolojia hii. Hadi Apple pia wamejiingiza katika utafiti wa utengenezaji wa teknolojia hii.
Inaonesha muda si mrefu utaweza kuingia kwenye gari, kuliambia unapoelekea na kisha wewe kutulia kwenye gari bila kujihusisha na uskani!!!! Unaoionaje hii? 🙂
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Mbunifu na mpenda teknolojia.
Muanzilishi wa Teknokona, TechMsaada na Teknokona Group LTD - WWW.TEKNOKONAGROUP.COM
Muda wangu umegawanyika kati ya kazi kibunifu @teknokonagroup na uandishi wa habari za Teknolojia hapa Teknokona Blog.
| mhariri(at)teknokona.co.tz |
One Comment
Comments are closed.