Dunia ya leo ni ya ushindani ambayo inapata msukumo mkubwa kutokana na ukuaji wa teknolojia unaopanuka kila sekunde. Washindani wa karibu sana kwa Apple kwenye biashara, Google wapo njiani kutoa Google Pay katika mfumo wa kadi.
Si dhambi kuiga kitu kizuri š š ambacho kitakuweka katika nafasi nzuri ya kuvutia watu hivyo basi kuweza kupata wateja wengi (wapya na wa zamani) kulingana na kile ambacho kinaweza kufanyika kwa kutumia bidhaa hiyo ambayo imeingia sokoni.
Google Pay ni nini?
Hii ni kadi ya kufanya malipo iliyotengenezwa na Google ambayo inakuwa imeunganishwa na akaunti yako ya benki itakayokuwezesha mteja kuweza kufanya malipo ya bidhaa kwa njia ya kidijiti hata kama ana salio (pesa) pungufu kisha kulipa deni wakati mwingine.
Kadi ya malipo ambayo itamuwezesha mtumiaji kuweza kufanya malipo ya bidhaa kupitia simu au kuchanja tuu.
Kadi hiyo imeshafanya makubaliano ya kibiashara na Mastercard, VISA pamoja na benki mbalimbali kurahisisha miamala kuweza kufanyika kiurahisi. Vilevile, Google Pay kwa sasa inamuwezesha mteja kuweza kufanya malipo mtandaoni bila shida yoyote lakini pia kumpa uwezo mtu kuifunga/kuzuia muamala ambao unatia shaka.
Mpangilio wa Google Pay katika mfumo wa kidijiti unawezesha miamala kufanyika bila ya kuhitaji kupitisha kadi kwenye mashine.
Uamuzi wa ujio wa kadi hiyo tafsiri ni kuendelea kuleta ushindani wa karibu kabisa kwa wapinzani wenzao ambao tayari wana Apple Card tangu Agosti 2019 lakini tofauti yao kubwa ikiwa kiasi ambacho mteja anaweza kutumia kufanya malipo ya bidhaa.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|