Baada ya kufanya uamuzi wa kugawanyika kibiashara mapema mwezi wa kumi (soma – Kampuni Ya HP kugawanyika!) kampuni ya HP imeleta kompyuta mpya ya kitofauti zaidi kutoka ya zote ambazo zimeshawahi kuingia sokoni. Nayo ni HP Sprout! Hii ni kompyuta ambayo imeenda kinyume na utamaduni wote wa ubunifu wa muonekano wa kompyuta wa zaidi ya miaka 35 ya utengenezaji wa kompyuta.
Je ina sifa gani?
Kwanza kabisa imefuta utumiaji wa kibodi (keyboard) kama tulivyozizoea. HP Sprout inakupa kajikamkeka (mat) cha kioo ambacho kina sensa za mguso (touch) hivyo kazi za kibodi na mausi zinachukuliwa na eneo hili. Kitu chochote utakachoandika au kuchora katika eneo hili kitakuwa pokelewa na kompyuta.
Pia kupitia kamera ya 3D iliyopo kwenye eneo la juu, kompyuta itaweza kupokea picha ya kitu chochote utakachoweka katika kajimkeka hako, yaani itapiga picha ya kitu/umbo husika, na utaweza kufanyia maboresha ya kiubunifu kwenye programu za ubunifu kwenye kompyuta.
Ukitoa uwezo wa skana (scanner), kompyuta hii pia inauwezo wa kutumiwa kama projekta. Sifa zote hizi ndani ya kompyuta moja inaifanya HP Sprout kuwa kompyuta ya kitofauti sana.
Swali kubwa ni je kompyuta hii ni kwa ajili ya watu gani na kwa matumizi gani?
HP wamesema hilo ni swali ambalo wao hawana majibu ya moja kwa moja nalo, wanategemea watumiaji kuweza kugundua wataitumiaje, lakini hadi sasa inaonekana ni kompyuta nzuri zaidi kwa wabunifu, watoto wanaopenda masuala ya sanaa kama uchoraji n.k. Lakini pia ilikuweza kuuza ata kwa watu wanaoitaji kibodi za kawaida ukinunua HP Sprout utapata kibodi na kipanya vya ‘wireless’, yaani visivyotumia waya ili kuweza kukusaidia kutotumia kamkeka ka mguso pale inapobidi.
Sifa Kuu
- Inakuja na Windows 8.1
- Kioo inchi 20
- Kioo/mkeka mguso inchi 23
- Prosesa Core i7 na Gb 8 ya RAM
Tazama video hii kutoka HP inayokutambulisha kwa HP Sprout. Kompyuta hii itauzwa kwa dola 1900 za kimarekani (takribani Tsh milioni 3.23), itaingia rasmi sokoni Novemba 9 mwaka huu.
Kumbuka Teknokona tunapatikana kupitia Twitter www.twitter.com/teknokona , Facebook www.facebook.com/teknokona na Instagram www.instagram.com/teknokona Ungana nasi leo 🙂
No Comment! Be the first one.