Katika siku kadhaa zilizopita kumekuwa na matangazo kadhaa hasa kwenye mitandao ya kijamii juu ya simu mpya inayouzwa kwa ushirikiano wa makampuni mawili nguli ya mawasilino nchini.
Simu hiyo inafahamika kwa jina la Huawei Y360 na imeingizwa sokoni kwa ushirikiano wa kampuni ya utengenezaji simu ya Huawei ambao na kampuni ya simu ya Tigo.

Baadhi ya watu maarufu wamekua wakiizungumzia kwenye kurasa zao binafsi. Kama unavyooa Dina Maris hapo juu. Kama mtandao wa masuala ya teknolojia, nikaona si mbaya kama tutaitazama simu husika, ili kujua kama YALIYOMO YAMO.
Kama unahitaji simu bora kwa gharama nafuu basi hii ni simu kwa ajili yako.
Simu hii inauzwa shilingi 160,000 kwenye maduka ya Tigo ambapo utarudishiwa pesa uliyonunulia kama vifurushi kwa miezi sita. Hii ni ofa nzuri sana kwa yeyote mwenye bajeti kali na anayetaka kumiliki simu janja ya Android yenye uwezo wa kutumia apps zote muhimu.
Sifa Kuu
Huawei Y360 inatumia Android OS, v4.4.4 (KitKat), kioo cha inchi nne na CPU Quad-core 1.2 GHz Cortex-A7. Ina kamera mbili, ya mbele (maalumu kwa SELFIE) ina 2MP na ya nyuma ina 5 MP, 2592 х 1944 pixels. Pia ina flash mbili kuweza kukusaidia kupata picha zenye ubora zaidi kwa mwanga sahihi..

Waswahili husema kizuri hakikosi kasoro, Je kuna kasoro gani nilizoona kwenye simu hii? Ukweli ni kwamba sikuona tatizo lolote hasa ukilinganisha na bei inayouziwa simu hiyo. Bei yake ni ndogo sana ukifananisha na sifa za simu hii.
Kwa maswali zaidi kuhusu upatikanaji wa simu hii unaweza wasiliana na Huawei Tanzania kupitia ukurasa wao wa Facebook, bofya-> http://on.fb.me/1QCgqrh
Kama unahitaji simu bora kwa gharama nafuu basi Huawei Y360 ni chaguo sahihi kwa sasa.
No Comment! Be the first one.