Inaamikika kuwa Samsung watazindua simu janja Galaxy Fold 8 kwenye tukio litakalofanyika Jumatano ya Julai, 22 2026 ambapo simu janja mbalimbali zinatazamiwa kuzinduliwa.
Imekuwa kama desturi ya Samsung kuzindua simu janja kwenye majira ya joto ambapo mwaka jana (2025) tukio kama hilo lilifanyika ambapo Samsung Galaxy Fold 7, Galaxy Z Flip 7. Inaaminika kuwa siku ya Jumatano (Julai 22) mwaka huu Galaxy Fold 8 pamoja na bidhaa nyinginezo kwenye hiyo familia zitazinduuliwa.
Katika tukio hilo ambalo litaruka mubashara kutoka jiji la London kuanzia saa 12 jioni saa za Afrka Mashariki (Tz, Kenya na Uganda) sawa na saa 3 asubuhi muda wa New York. Kwenye tukio inategemewa bidhaa kama Z Fold 8 Ultra itazinduliwa pia ikitazamiwa kuwa na muonekano sawa na Z Fold 7 iliyotoka mwaka 2025. Halikadhalika, pengine tukashuhudia ujio wa toleo jipya la saa, miwani janja za Samsung.
Tukio hilo litakuwa mubashara na mengine tutaweza kuyafahamu Julai, 22 2026 na hapo haitakuwa fununu tena bali habari za uhakika kutoka kwa wahusika. Je, ungependa kufuatilia matangazo hayo mubashara? Kama jibu ni ndio basi utaweza kufuatilia kupitia chaneli hii pale YouTube.
Vyanzo: The Verge, CNET
No Comment! Be the first one.