Kampuni ya simu za mkononi Infinix hivi majuzi ilizindua Infinix HOT 30 kwa nchi za ughaibuni. Sasa, inajiandaa kuzindua Infinix HOT 30 nchini Tanzania.
Infinix kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii @infinixmobiletz inaashiria ujio wa simu hiyo – Infinix Hot 30 — Aprili 25 ya mwaka huu.
Kwa mujibu wa tovuti mbalimbali duniani kama GIZMOCHINA, KLGadgetTV na nyenginezo zimedai kuwa Infinix HOT 30 inaufanisi wa hali ya juu.
Hivyo inaelezwa kuwa soko la simu za kima cha kati kuja kuwa hatarini. Infinix HOT 30 imeudwa na kichakataji chenye misingi 8 cha MediaTek Helio G88 (prosesa).
Bila kusahau ikiwa na core mbili kali za ARM Cortex A75 na 2.0GHz, inahakikisha uchezaji laini wa games mitandaoni na hata zile za bila mtandao.
Kwa kuongeza, nguvu ya battery ya mAh5000 yenye kuhimili utumizi wa muda mrefu pasipo kuishiwa moto kiholela kunaipa hadhi HOT 30 kuwa simu bora zaidi kwa mwenye kipato cha kati.
HOT 30 inasemekana kuwa na uwezo wa kuongeza ufanisi wa kumbukumbu/Memory kutoka Ram ya GB8 hadi 16GB ili kuwezesha uanzishaji wa haraka wa michezo/magemu na kufanya kazi nyingi kwa kasi ya hali ya juu.
Kama haitoshi pia inasadikika kioo cha HOT 30 ni smooth/laini zaidi wakati wa utumiaji kimeudwa na refreshrate 90Hz, touch rate 270 na teknolojia ya uboreshaji eneo la giza DRE inasemekana HOT 30 ni simu ya pekee kuwahi kuwepo kwenye muendelezo (series) ya simu hizi.
Kwa sifa hizi za haraka haraka ambazo tumezipata katika vyanzo vya kuaminika inaonyesha dhahiri kwa kifaa hichi ni cha aina yake na kitakua na nafasi nzuri sana katika soko.
Kuhusu bei na sifa nyengine za simu hii tembelea @infinixmobiletz mara kwa mara.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je unaonaje kuhusiana na jambo jhili? Tutazidi kukupa taarifa juu ya simu mara baada ya kuzinduliwa tarehe 25 kwa hapa Tanzania.
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.