Infinix ni moja ya makampuni makubwa katika utengenezaji wa vifaa vya teknolojia na imejikita sana katika soko la simu janja, ni moja ya makampuni makubwa kimauzo nchini Tanzania na hata kwenye mataifa mengine Afrika.
Safari hii katika soko wanakuja na matoleo ya Hot 70 ambayo yatakua na teknolojia ya hali juu na huku moja ya matoleo yakitegemewa kuwa na uwezo wa kubadilika rangi kutokana na aina tofauti ya joto.
Naam, ushawahi kuona simu yenye uwezo wa kubadilika kulingana na mabadiliko ya hali ilipo? Jibu unalo mwenyewe!
Rangi hiyo inaweza kubadilikabadilika kulingana na hali ya joto, ni wazi kwamba vifaa vya kiteknolojia vinaweza kupata joto kwa sababu nyingi tuu – utendaji kazi au eneo ambalo mtumiaji ameiweka.
Kwa sasa matoleo haya ya Hot 70 hatuna uhakika yatakuja mangapi maana hata katika mitandao ya kijamii ya Infinix bado hayajawekwa wazi.
Kwa matoleo yalitopita ya Infinix Hot 60 yalikua ni manne hivyo basi kwa matoleo ya Hot 70 namba hiyo inaweza ikashuka, ikapanda au hata kuwa sawa. Tutajua zaidi wiki ijayo.
Tetesi nyingi zinaashiria kwamba simu hii itakuja katika rangi tofauti tofauti lakini inayosubiriwa kwa hamu na kwa uhakika ni rangi ya chungwa / orange.
Katika matoleo hayo toleo la chini kabisa (Hot 70) linaweza likaja na Media Tek Helio G99 SoC huku RAM yake ikiwa na ujazo wa 4GB.
Fununu zingine zinaeleza kwamba toleo la Hot 70 pekee litakuja katika aina mbili huku aina hizo zikiwa zinatofautiana uwezo wake wa betri.

Kaa nasi kwani endapo tukipata taarifa Rasmi kuhusiana na simu hizi, tutakuwa wa kwanza kukufikishia.
Wewe unavyohisi simu hii itakuja na kipengele (feature) gani kali ambayo itaifoutisha na simu nyingine katika soko?
Inategemewa Hot 70 itazinduliwa rasmi wiki ijao kwa hapa Tanzania, hivyo tukae mkao wa kuipokea

No Comment! Be the first one.