Kila mwaka Apple hutuonyesha simu mpya ya “Pro” inayovutia macho, lakini safari hii inaonekana walipiga msasa upande mmoja na wakasahau mwingine. iPhone 17 Pro na Pro Max zimeingia sokoni wiki hii, na tayari mitandaoni kumejaa malalamiko: simu inakwaruzika kirahisi sana kwenye sehemu ya bump ya kamera.

Tatizo Liko Wapi?
Kwenye kona zile kali za kamera. Zack Nelson (JerryRigEverything) alifanya jaribio na kugundua kuwa aluminium coating haishikii vizuri kwenye kona, na mara tu sarafu au funguo zikigusana, rangi inachubuka. Hii siyo issue mpya – ni udhaifu wa kimuundo kwenye mchakato wa anodizing.
Kwa maneno mengine: simu yako mpya inashindana na funguo mfukoni, na funguo zinaibuka mshindi.
Mashabiki Wameliona Mapema
Bloomberg imeripoti kuwa hata kwenye Apple Stores, simu za maonyesho zilianza kuonyesha mikwaruzo baada ya saa chache tu.
-
Rangi ya Deep Blue iPhone 17 Pro ndiyo imeathirika zaidi.
-
Black iPhone Air pia imekuwa na doa mapema sana.
Kwa kifupi, simu mpya kabisa inaweza kuonekana “imepitia mengi” ndani ya siku moja tu.

Linganisho na iPhone 16 Pro
Mashabiki wanakumbuka mwaka jana:
-
iPhone 16 Pro ilikuwa na mwili wa titaniamu uliosifiwa kwa uimara.
-
Camera bump yake ilikuwa na mpini (radius) uliosaidia kupunguza mikwaruzo.
Ukweli mchungu ni kwamba iPhone 17 Pro inaonekana imeshinda upande wa muonekano – lakini imepoteza kidogo upande wa uimara.
Je, Apple Walipanga Hivi?
Inawezekana kabisa. Kwa macho, kona hizo kali zinafanya simu ionekane ya kifahari zaidi. Lakini kwa mmiliki, inamaanisha ama ununue jalada mara moja, ama ukubali simu yako ionekane na “patina” mapema.

Ushauri wa Haraka
-
Tumia case yenye ulinzi wa kamera.
-
Epuka kuweka simu mfukoni na funguo.
-
Ukipenda rangi, zingatia rangi nyepesi – zinabeba mikwaruzo kwa siri zaidi.
Hitimisho
Apple imeleta simu nzuri, nyepesi na ya kifahari. Lakini kama ulitarajia uimara kama ule wa iPhone 16 Pro, basi utalazimika kuishi na mikwaruzo, au kukaa na jalada 24/7.
No Comment! Be the first one.