Wakati Apple ilipozindua iPhone 17 Series, mashabiki wengi walitarajia kupata simu yenye kamera bora zaidi, betri inayodumu muda mrefu, na chipu za nguvu ya kipekee. Hakika, maboresho haya yapo. Lakini jambo lililoibua hasira na mijadala mitandaoni siyo uwezo wa ndani ya simu — bali muundo wake mpya.
Kwa mara ya kwanza, Apple imebadilisha kabisa sura ya kifaa, hasa iPhone 17 Pro na Pro Max, ambazo sasa zina bar ya kamera inayochukua sehemu kubwa ya juu ya kifaa. Badala ya kushangiliwa, hatua hii imezua hisia mchanganyiko: wapenzi wa Apple wamelalamika, wengine wacheka, na wengi wameonyesha kutoridhishwa mtandaoni.

Kwa Nini Muundo Mpya Umelalamikiwa
Apple imejijengea jina kwa muundo wake wa kifahari na minimalist. Lakini kwa watumiaji wengi, iPhone 17 sasa inaonekana kama simu za Android — jambo ambalo Apple iliwahi kukejeli hapo awali. Wengi wanaona mabadiliko haya kama kuvunjika kwa urithi wa Steve Jobs, ambaye aliheshimu urahisi na muonekano safi.
Kamera “Bar” Iliyoibua Hisia
iPhone 17 Pro na Pro Max zinakuja na “full-width camera island”, bar inayochukua karibu theluthi ya sehemu ya juu. Lengo la Apple lilikuwa urahisi wa kuchaji bila waya na muonekano wa kisasa. Lakini mashabiki wanasema ni kuzusha migogoro ya muundo.
Mfano kutoka X/Twitter, Daniel Spencer (@DanielSpencer) aliandika:
“The iPhone 17 Pro is ugly and it looks like an Android.”
Tafsiri: “iPhone 17 Pro ni mbaya na inaonekana kama Android.”
Enzi za Steve Jobs Zikumbukwa
Mashabiki wengi walionyesha kuwa Apple imepoteza mwelekeo wa urahisi wa muundo uliokuwa dhahiri enzi za Steve Jobs.
Mfano kutoka Reddit, Sumit Behal, alisema:
“This is the ugliest iPhone ever. Steve Jobs would have fired everyone in his era.”
Tafsiri: “Hii ndiyo iPhone mbaya zaidi kuwahi kutengenezwa. Steve Jobs angefukuza wote enzi zake.”

Kutofautisha na Android
Muundo wa bar ya kamera umelinganishwa na Google Pixel 10, jambo lililoleta mjadala mtandaoni. Mtumiaji mmoja aliandika kwenye X (chanzo: New York Post):
“This used to be the s–t Apple mocked other phone companies for, and here they are becoming a parody of themselves.”
Tafsiri: “Hivi ndivyo Apple ilivyokuwa ikiwadhihaki wengine, sasa wao wenyewe wamekuwa kejeli ya kampuni yao.”
Rangi Zilizozua Mjadala
Mbali na muundo wa kamera, chaguzi za rangi pia zimevutia hisia mchanganyiko. iPhone 17 Pro na Pro Max zinapatikana kwa silver, deep blue, na cosmic orange, bila chaguo la black. Mashabiki waliiona kama kuondolewa kwa rangi ya jadi ni kosa kubwa.
Mwanakriti wa teknolojia, Sebastiaan de With (@sdw) aliandika:
“No black iPhone 17 Pro is just insanely dumb. Black phone people in shambles.”
Tafsiri: “Kutokuwa na iPhone 17 Pro ya rangi nyeusi ni upuuzi mkubwa. Mashabiki wa simu nyeusi wako hoi.”
Wengine walichukulia rangi ya machungwa kama dhihaka kwa wateja. Mtumiaji mwingine, @agentg, alisema:
“iPhone 17 Pro, our ugliest iPhone ever #AppleEvent”
Tafsiri: “iPhone 17 Pro, iPhone mbaya zaidi kuwahi kuwepo #AppleEvent.”
Hitimisho
Kizazi cha iPhone 17 kimeonyesha wazi kuwa Apple haiko tayari kukaa kimya. Teknolojia ya ndani ni ya kushangaza, lakini muundo umegeuka kuwa mada ya mgawanyiko. Mashabiki wa Apple sasa wanajiuliza: je, hii ni mwanzo wa enzi mpya ya ujasiri wa Apple, au kosa kubwa litakalokosa kuridhisha wafuasi wake waaminifu?

No Comment! Be the first one.