Wikipedia ni sehemu ambayo mtu yeyote anaweza kujiandikisha na kisha kuandika kitu/vitu kuhusu topiki fulani. www.wikipedia.org inatumia mfumo wa wiki —Yaani mtu yeyote anaweza andika kitu katika mitandao hiyo—
Mara nyingi mambo yanayoandikwa katika wiki/wikipedia yanakuwa ni ya ukweli lakini hata baadhi ya muda yanakuwa yana chembe chembe za uwongo kwani kila mtu anaweza andika lolote katika ukurasa huo huo mmoja
Hivi ushawahi kujiuliza ni nani au ni kitu gani ambacho kinahaririwa sana katika mtandao wa wikipedia? Mtandao wa wikipedia mpaka sasa una makala zaidi ya 4,964,779 za kiingereza tuu na makala milioni 35 katika lugha 288 tofauti tofauti (ambazo sio katika lugha ya kiingereza).
Kurasa mpaka ijichukulie umaarufu wa kuhaririwa sana ni lazima iwe na mambo mapya yanayojitokeza mara kwa mara sio? ndio! lakini unaweza shangaa hata kurasa ambazo hazina taarifa mpya (za kale) zinapata kuhaririwa sana.
Katika utafiti uliofanywa na Bw. Ramiro Gómez, ambae ni ‘developer’ wa ‘sofware’ anaekaa Berlin, umekuja na majibu ya swali letu juu ya kurasa zipi zinahaririwa sana katika wikipedia. Bw Ramiro Gómez alitumia mda wake katika kukusanya taarifa mbalimbali juu ya jambo hili
Mpaka sasa anaeongoza kuhaririwa sana ni raisi mstaafu wa marekani Bw. George W. Bush. Unaweza pia shangaa licha ya listi kuwa na Timu za michezo/wanamichezo kama vile Real madrid, Roger Federer na kuwa na Michezo ya Video kama vile PlayStation 3 na RuneScape lakini mwanamke ni mmoja tuu Britney Spears, ambaye amejitokeza katika list hii ya watu/vitu 30 vinavyoongoza kuhaririwa katika mtandao wa wikipedia
Pata Habari Picha Juu Ya Kurasa Zinazoongoza Kuhaririwa Katika Wikipedia!

No Comment! Be the first one.