Kuna njia mbalimbali za kuroot simu hasa hasa za Android lakini ni njia chache sana zinafanya kazi hiyo kwa urahisi zaidi kama Kingo Root.
Kingo Root ni programu unayoweza kutumia kwenye kompyuta na pia hata kwa kutumia simu yako tuu.
Programu tumishi ya kuroot simu za Android. Kuroot Android 6/6.0.1 bofya>>HAPA
Faida za kuroot simu.
Kiuhalisia zipo sababu nyingi tu za kwanini ni muhimu wa kuifanya simu yako iwe ya kitofauti na vile ambavyo uliinunua lakini daima kuna vile vitu ambavyo vinasababisha utake kuijua simu yako kiundani zaidi:
Kuwa na uwanja mpana wa kutumia simu. Unapofanya maamuzi ya kuroot simu basi ni dhahiri kuwa utakuwa umejiweka katika nafasi nzuri kuweza kuvifikia vipengele vya ndani zaidi ambavyo vitakufanya uweze kuitumia simu yako kwa uhuru zaidi.
Kwa simu ambayo imeshafunguliwa kiundani zaidi inakupa uwezo wa kuamuru programu tumishi yoyote ambayo ipo tayari kwenye simu/unataka kuipakua kutoka kwenye Play Store.
Simu ambayo inaweza kutumiwa kimapana zaidi inakupa uwezo wa kuhamisha hata zile programu tumishi ambazo kikawaida haiwezekani kuzihamisha kutoka sehemu moja hadi nyingine.
Masasisho. Simu ya namna hii haisubiri masasisho mpaka simu nyingine za Android zipate ndio na yenyewe ipate, la hasha! Bali simu ambazo zimeshafunguliwa kimapana zaidi zinapokea masasisho mapema kabisa bila ya kusubiri chochote.
Wahusika wa kuleta masasisho kwenye simu huwa wanatoa maboresho hayo kwa simu ambazo zinatumiwa kwa uhuru zaidi (rooted).
Ufanisi wa simu. Kwa simu ambayo ipo katika ngazi hii ya ubora inakuwa ni nyepesi katika ufanyaji wake wa kazi na hata kuweza kuifanya betri liweze kutunza chaji kwa muda mrefu kutokana na kwamba unaweza ukaifikia mipangilio mingi zaidi ndani ya simu husika.
Muhimu – Hakikisha kabla haujaribu kufanya hili uwe umesoma makala yetu inayoelezea zaidi kuhusu suala la kuroot simu za Android – Nini maana ya kuroot simu ya Android!.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|