Lenovo ni moja kati ya kampuni la kiteknolojia linalofanya vizuri sana katika soko, kampuni hili linajulikana sana kwa ubora wake katika soko la simu janja na kompyuta.
Lenovo wao kwa sasa kuna aina za simu ambazo wao wamezipiga chini hali ya kwamba imewashangaza wengi.

Simu hizo zilikua zimepewa jina la “Legion Mobile Gaming Phones’ na lengo lake kubwa ilikua ni kujitenga na simu janja za kawaida katika kampuni hiyo na kuhakikisha bidhaa hii inajitegemea.

Kingine cha kukiweka akilini ni kwamba kampuni hiyo haijatangazwa kwamba inaacha kabisa kujihusisha na maswala ya magemu… kumbuka saa nyingine maamuzi kama haya ndio huwa yanapelekea kampuni kuja na njia nzuri zaidi (labda ya kufurahia magemu).
Kumbuka simu janja ambazo zipo mahususi kwa ajili ya magemu zipo nyingi tuu hivyo Lenovo hakuwa peke yake katika soko.. kuna kampuni kama ASUS, Xiomi, Nubia Red Magic na nyingine nyingi zilikua na vifaa vya aina hii katika soko.

Ningependa kusikia kutoka kwako, unadhani Lenovo pengine wanataka kuja na kifaa kingine cha kucheza gemu kama vile Playstation?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.