Makaburi matatu yanayotembelewa sana na watu jijini Moscow yawekewa huduma ya intaneti/mtandao ya wi-fi. BUREEEE
Makaburi hayo yanayotembelewa sana, wanaotembelea wataweza kutumia mtandao wa intaneti bila malipo katika makaburi ya Novodevichy, Troyekurovskoye na Vagankovo na huduma hiyo ilianza mapema mwaka huu kwa mujibu wa tovuti ya Moscow City.
Mkuu wa huduma za makaburi mjini Moscow Bw. Artem Yekimov anasema lengo ni kusaidia wageni kwenye makaburi hayo kutafuta habari zaidi kuhusu watu mashuhuri waliozikwa humo. Aidha, kuwafanya wafurahie matembezi yao makaburini.
Kampuni ya mawasiliano ya “YS System” inasema ilijitolea kuweka huduma ya wi-fi humo baada ya kusikia mipango ya kutenga maeneo ya watu “kutulia kisaikolojia” katika makaburi hayo.
Makaburi ya Novodevichy ni moja ya maeneo yanayotembelewa sana na watalii Moscow. Miongoni mwa watu waliozikwa humo ni mwandishi Anton Chekhov, kiongozi wa zamani wa muungano wa Usovieti (USSR) Nikita Khrushchev na rais wa zamani wa Urusi Boris Yeltsin.
Soma Pia – Makanisa Kuwekwa WiFi nchini Ujerumani