Ni wazi kwamba china ni moja kati ya soko kubwa kabisa katika maswala mazima ya kutengeneza na kuuza simu.
Simu nyingi huwa zinauzika sana na mara nyingi soko hilo ni gumu maana bidhaa nyingi ambazo zinauzika basi asilimia kubwa zinatoka hapo hapo china au nchi zingine za bara la asia.
Kumbuka makampuni haya yapo katika maongozi ya kuwezesha jambo hili baada ya kuona kabisa linawezekana na mfano mzuri wameupata baada ya Huawei kuja na harmonyOS.
harmonyOS ilikuja na wengi waliipokea vizuri huku watu wengi mwanzoni kabisa waliona kuwa haitopata heshima kama ilvyotarajiwa vile vile wengi walikua wanaibeza maana ilikua inashindana moja kwa moja na Android.
Kingine ni kwamba makampuni haya yanafanya hivi ili kuhakikisha kuwa wanaliendesha soko lao wenyewe kama wenyewe maana simu ni zao (asilimia kubwa) lakini programu endheshi ni za wamarekani.
Soko la China ni moja kati ya soko gumu sana kwa teknolojia ya marekani ndio maana vitu vingi huwa havipatikani kwa urahisi kama katika mataifa mengine.
Mpaka sasa inasemekana vifaa milioni 700 vya Huawei vinatumia HarmonyOS na hii ni kwa china pekee ukiachana na nchi zingine.
Kingine ni kwamba makampuni mengi ya simu nchini humo bado yanatumia mfumo wa uendeshaji wa vifaa vyao wa Android lakini haimaanishi kwamba hilo halitakuja kubadilika.
Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika uwanja wa comment, je hili umelipokeaje? Je unshauri kampuni hizo kuja na njia moja au kubaki katika Android tuu?
Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.
Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii
Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn
No Comment! Be the first one.