Wiki iliyopita niliweka hapa habari kuhusu simu mpya za Huawei aina ya Huawei Y360. Kama ulikosa habari ile, kwa kifupi ni kuwa makampuni makubwa ya simu za mkononi za Huawei na TIGO wameungana na kuleta simu nchini ambazo zinauzwa kwa bei nafuu ya shilingi 160,000 pekee kwenye maduka ya Tigo nchi nzima huku ukirusishiwa pesa uliynunulia kama vifurushi.
Wiki hii nisingependa kuzungumzia simu tena, ila ni maoni ya Watanzania wa kawaida watumiaje na wasio watumiaji wa simu kuhusu habari ile. Nimekukusanyia maoni hayo hapa chini.
“Baada ya kusoma habari yako, nimenunua simu hii kwenye duka la Tigo Temeke, ni kweli kama ulivyosema, wamenirudishia pesa kama vifurushi ”
Nassoro, Temeke
.
“Simu ni nzuri sana, hasa kamera yake ndio nimependa na bei yake sio kubwa, wamejitahidi”
Tekla, Dodoma
..
“Watu wamezichangamkia sana inaonekana, maana siku ya kwanza nimeenda nimekuta foleni watu wananunua. Ni simu nzuri na picha zake nzuri ”
Mariam, Mbeya
No Comment! Be the first one.