Kuanzia jumatatu huduma za Blackberry zimekuwa na matatizo katika nchi nyingi duniani pamoja na Tanzania, kwa habari za uhakika ni kwamba huduma zimeshaanza kurudi katika hali ya kawaida kwa watumiaji wengi ingawa bado kutakuwa na matatizo mengine yatakuwapo bado. Asa kwa watumiaji wa nchi za Ulaya, Uarabuni, India na Africa [Nchi zinazotumia network ya mfumo wa EMEIA.
Ila kwa uhakika zaidi ni kwamba huduma ya Barua Pepe [Email] ndo ipo imara tayari, ila kwa Web Browsing ambayo ni hasa hasa kwa utumiaji wa intaneti bado itakuwa si ya uhakika kwa watumiaji wengi.
Je ni nini kilichotokea?
Imeelezwa ya kuwa matatizo yametokea Europe na kusambaa,limesababishwa na matatizo katika kifaa cha kompyuta kinachoitwa Servers. Hichi ndo kinasimamia huduma zote za internet kwa watumiaji wa Blackberry.
Kwa ushindani wa huduma kwa sasa, kutoka kwa simu nyingi nzuri za Android na Iphone mpya wiki hii kunawafanya wachambuzi wengi kuamini kuwa Blackberry wanaitaji kuwa waangalifu zaidi!
No Comment! Be the first one.