Katika miaka ya karibuni matumizi ya akili mnemba ni maarufu duniani kote; si kwa wanafunzi, wafanyakazi hata wazee ikiwa kama chombo ambacho kina uwezo wa kutoa majibu kwa kile utakachouliza na ChatGPT ni marufu sana kuliko akili mnemba nyingi tuu kama sio zote ambazo zinatumika.
Mara zote mtu anapotumia akili mnemba/unde baada ya kutoa majibu ya kile ambacho mtumiaji ameuliza mwisho kabisa utakutana na angalizo la kwamba kuna uwezekano majibu husika yasiwe sahihi basi ni vyema mtu akafanya uchunguzi zaidi. ChatGPT ina watumiaji wengi tuu duniani kote lakini kampuni inayomiliki bidhaa hiyo imesdhtakiwa mahakamani kutokana na ushauri uliohusu masuala ya afya kiasi kwamba karinu mtu apoteze uhai.
Mchungaji aishtaki OpenAI kutokana na kile ambacho ChatGPT ilimpa kama jibu kwa kupendekeza vitu hatari zaidi kuhusiana na kile ambacho mchungaji aliuliza ChatGPT. Swali lake lilihusiana na masuala ya afya. Kutokanana na ushauri huo ilisababisha mchungaji kuchelewa kupata huduma stahiki. Aliyelalamikiwa ameeleza inasadikiwa (allegedly) dalili alizoziainisha hazikuwa za hatari na kuongeza kuwa ChatGPT ilienda mbali zaidi kwa kutoa jibu kulingana na imani ya mchungaji kwamba “Mungu hakuumba mwili wako ili uendelelee kushindwa bila kikomo“~tafsiri isiyo rasmi.
Inasadikika kuwa akili mnemba ilimshauri kutosikiliza ushauri kutoka kwa marafiki/familia wa kwenda hospitali. Inaelezwa kuwa mchungaji aliifungukia akili mnemba kuwa waumini wake kanisani wanamuona hana akili kwa kutokwenda hospitalini kutafuta matibabu. Akili unde ikamjibu kwamba “…watu wengi wakiwemo (waumini wapenda mema) huwa hawaelewi tuu“.
Mchungaji ameenda mahakamani kutaka kulipwa fidia lakini pia kuomba ChatGPT Health izuiliwe kutoa ushauri/majibu kuhusiana na masuala ya afya mpaka pale watu wasiofungamana upande wowote wafanye upembuzi yakinifu na kutoa majibu kuwa mfumo huo ni salama kutumia. Inaelezwa kuwa karibu watu 230M kila juma wanatumia mfumo huo kwa kupandisha nyaraka zao za afya ili kupata usaidizi/ushauri kutoka ChatGPT.
Vyanzo: Engadget, The New York Times.
No Comment! Be the first one.