METAVERSE! Nitakwambia kitu kimoja. Hii inakuja na inakuja kuwa sehemu ya maisha yetu kama ilivyo internet, na itakuwa vyema kama ungetumia mda wako kuielewa.
Kwa watu wenye shauku na teknolojia wamesikia/kusoma kuhusiana na Metaverse. Unakumbuka stori za babu/bibi kule kijijini mkiwa mmezunguka moto? Ilikuwa kipindi kizuri miaka ile stori za kusogeza muda bila runinga wala simu na maisha yalienda vizuri tuu.
Vile vikundi vichache vya watu havikuwa vinatosha, Binadamu tunapenda kuhusiana na watu wengi zaidi na kujifunza tamaduni za jamii tofauti na zetu, ikaletwa internet miaka ya mwisho ya 1980. Ukuaji wa internet ukapelekea dunia kuanza kuwa kijiji kimoja.
Barua ziligeuka kuwa barua za kielektroniki. Dakika chache zilitosha kuandika na kutuma ujumbe wa kieletroniki kutoka Tanzania kwenda Marekani. Bado haikutosha tulihitaji kuwa na marafiki wengi zaidi kutoka maeneo mbali mbali. Ikaja mitandao ya kijamii kama Myspace, Friendster na Facebook.
Hii yote ni jitihada za binadamu kutaka kuwa pamoja kwa namna yoyote bila kujali umbali kati yao. Watu wengi wametamani kuwepo Marekani au Ulaya, lakini imeshindikana kwa sababu tofauti tofauti. Mitandao ya kijamii imekuja kurahisisha kidogo hili jambo.

Leo kwa kuangalia picha, Google Maps au video mtandaoni unajua Paris, Ufaransa ilivyo, Majiji makubwa kama Las Vegas, California, Tokyo, London na Dubai unayajua kama vile umewahi kuishi huko sababu Mitandao ya kijamii imekupa nafasi ya kuishi katika majiji hayo kidijitali. Hivi umewahi kufikiria sikumoja kwamba unaweza kwenda sehemu fulani bila kupanda gari, ndege au usafiri wowote na ukafika?
Metaverse inafanya tuishi ndani ya mitandao na sio kuona tu kama ilivyo sasa. Maana yake ni kwamba badala ya wewe kusoma hili andiko kama unavyofanya sasa, mimi na wewe tutakaa pamoja kidijitali na hii elimu kwa sauti teknolojia hii inawezesha kuuliza maswali yako moja kwa moja kwa sauti, Inawezekana ukawa ni mtu usiyependa kuonekana kwa sura yako halisi mtandaoni. Usihofu Metaverse itazingatia hilo Ndani ya Metaverse unachagua unataka kuonekana vipi kwa watu wengine.
Mfano unaweza kuchagua kuonekana kama roboti au kiumbe yeyote wa ajabu. Ni vyovyote vile nitakavyotaka. Ushawahi tamani kukutana na rafiki zako uliosoma nao ila mnashindwa kwa sababu ya kukosa muda na mko sehemu tofauti tofauti?. Ndani ya Metaverse utaweza ruka toka sehemu moja kwenda nyingine ndani ya sekunde tu, Hivyo mnaweza kukubaliana kukutana sehemu yoyote ndani ya huu ulimwengu wa kidijitali na wote mtakuwepo bila kusafiri katika ulimwengu wa kweli.
Kuna makumpuni ambayo tayari yameanza kutengeneza Metaverse. Kuna Microsoft, Google,Apple na Facebook (sasa wanaitwa META), wote wameanza kutengeneza Metaverse.
Je, Metaverse ni kama mitandao ya sasa kwamba inamilikiwa na mtu/kampuni moja kila moja kivyake?
Bw. Mark Zuckerberg alisema kwamba kuna nafasi ndogo sana ya kila kampuni kumiliki Metaverse yake yenyewe. Metaverse ni kama internet haiwezi kumilikiwa na mtu au kampuni moja. Kwa maana hiyo Metaverse sio bidhaa moja au kifaa kitakacho milikiwa na mtu mmoja. Hiyo ni kulingana na muanzilishi wa Facebook, M. Zuckerberg
Katika kutengeneza ulimwengu ambao utakuwepo mtandaoni Facebook na Microsoft wametia nguvu kubwa sana, Facebook wamepanga kuwekeza $10 Billion katika kutengeneza Metaverse. Vile ambavyo mitandao ya kijamii imetuunganisha kuweza badilishana mawazo kutoka popote tulipo duniani basi na Metaverse itakuwa vivyo hivyo, ila katika ubora zaidi. Kama ulipoanza kupost mambo yako Twitter, Instagram au facebook ndivyo utakavyoanza kwenye metaverse. Kule hautakuwa unapost. Ndani ya metaverse utakuwa unakusanya vitu, kujenga na kuongea na rafiki zako moja kwa moja kama kikao cha familia.
Wadau wa sarafu za kidijitali wanaweza kukubaliana na sisi kwamba inaweza kuwa ni vyema ukaanza wekeza katika sarafu ambao hapo baadae zitatumika katika ulimwengu wa Metaverse. Sarafu hizo ni kama Decendraland (MANA) na SAND. Hii ni kwa sababu, iwapo metaverse itakuwa haimilikiwi na mtu mmoja (decentralized) basi tutahitaji pesa za kutumia ndani ya huo ulimwengu, Labda njia za malipo zilizopo kama paypal zitafaa. Hapana, haziwezi kufaa sababu sarafu za Serikali hutofautiana kila nchi.
No Comment! Be the first one.