Microsoft imejikita katika kuingia katika makubaliano ili kupata ushirikiano wa Dell pamoja na hewlett packard (HP) katika kuuza tabiti zake zinazojulikana kama Surface Pro kwa wateja wakubwa (makampuni).
Katika makubaliano hayo kampuni la dell litatumia kitengo chake cha mauzo, kuuza tabiti hizo za microsoft na vifaa kuanzia mwezi oktoba. Pia itawezekana hata kwa biashara hizo kununua tabiti za surface pro katika mtandao wa dell.
Habari hizi zinakuja baada ya soko la tabiti kuonyesha kushuka. kila mtu anaangalia atafanikiwa vipi kupata mauzo makubwa ya tabiti. Hata Apple wamefanya maboresho makubwa ya tabiti zao (iPad) ili mradi tuu wapate mauzo yanayoridhisha. Japokuwa microsoft ilipata mauzo makubwa tuu katika kuuza tabiti zao lakini bado wanataka kupata zaidi
Dhumuni kubwa la microfort ni kwamba lini malengo ya kupata zaidi (faida) kupitia makampuni makubwa ambayo yatanunua tabiti hizo kwa wingi na kwa pamoja . Lakini pengine labda kampuni hili linafanya hivi baada ya kusikia kuwa Apple wapo mzigoni kuja na iPad mpya
Kampuni la microsoft sio la kwanza kuingia katika makubaliano na kampuni lingine kwa lengo la kuuziwa tabiti zake. Kampuni ya Apple na yenyewe iliingia mkataba mwezi agosti na kampuni ya CISCO ili iuzie tabiti zake kwa biashara kubwa (makampuni). Licha ya hivyo pia kampuni imeingia mkataba na kampuni la IBM ikiwa na lengo kampuni hiyo (IBM) iwatemgemezee Apps zitakazo tumika katika biashara (Kama vile kwa makampuni)
Maelezo kuhusiana na ushirikiano wa microsoft na Hewlett Packard bado haujawa wazi, lakini unaweza kushangaa ukawa kama ule ule unaofanana na Dell tuu.
No Comment! Be the first one.