Simu janja zimekuwa lukuki na zina muonekano na ukubwa ambao unafanana na rununu mbalimbali lakini sasa kuna hii Mony Mint ambayo ni ndogo zaidi na ilitoka mwaka 2021.
Kwenye teknolojia ya ;eo matumizi ya simu janja si jambo la ajabu wala la anasa. Katika pitapita zangu nikakutana na Mony Mint; simu janja ambayo ni ndogo inayoenea kwenye kiganja cha mkono. Ni simu janja ambayo inatumia teknolojia ya 4G. Mbali na kuwa na kutosha kwenye kiganja cha mkono tu ina sifa hizi:
Muonekano|Kipuri mama
Hapa tunakutana na simu janja yenye kioo cha urefu wa inchi 3 LCD, 480x854px. Ina kamera ya mbele ya ina uwezo wa kuchukua picha/video wa 480p. Kipuri mama ni cha kwenye simu hii ya uwezo wa kati – Mediatek MT6735: Quad-core CPU (4×1.3 GHz Cortex-A53).
Memori|Betri/Bei
Kwenye kipengele hiki tunakutana na RAM ya GB 3 kwa 32GB. Upande wa betri simu hii ina 1250mAh. Bei yake ni $150 ambayo ni sawa na Tsh. 344,400 (2021).
Kamera|Mengineyo
Simu hii ina jumla ya kamera yenye MP 13, ina uwezo wa kurekodi video ya ubora wa 480p, Inatumia Android 9, ina uwezo wa kuweka memori ya nje. Wengi wanauliza kwanini iwe ndogo kiasi hiki? Jibu la Mony (walioitengeneza) wanasema ni kutokana na kwamba matumizi ya simu nzito haivutii.
Mony Mint ni simu ambayo inafaa kwa matumizi ya kawaida kabisa na kwa wale ambao wanapenda kubemba rununu ambazo si nzito na zenye muonekano mzuri.
VyanzoL GSMArena, mitandao mbalimbali
No Comment! Be the first one.