Tunafahamu vyema Intenet Explorer haipo tena kwenye ulimwengu wa matumizi. Ni jambo jema kufahamu ya kwamba sifa ya kivinjari cha kwanza kuwezesha rangi na picha kuonekana vizuri kabisa bila shida yoyote.
Kivinjari cha NCSA Mosaic ndio kinashikilia rekodi na kutambulika kama kivinjari cha kwanza duniani kuwezesha watumiaji wake kutumia mfumo wa intaneti wa kisasa. Kivinjari hiki ndio kilipaisha teknolojia ya World Wide Web (www) iliyotengenezwa na Bw. Tim Berners-Lee mwaka 1990.
Kabla ya kivinjari cha Mosaic vilikuwepo vingine huko nyuma lakini hiki (NCSA Mosaic) ni cha kwanza kwa sababu kilikuwa na muonekano wa kuvutia kwa maana ya kwamba kuwa na rangi mbalimbali pamoja na picha. Kivinjari cha Mosaic kilitengenezwa na timu ya wanafunzi iliyoongozwa na Bw. Marc Andreessen pale Chuo Kikuu cha Illinois-Urbana-Champaign.
Toleo la kwanza la kivinjari hiki tayari kilikuwa na vitu muhimu ambavyo vinajieleza vyenyewe kwa mtumiaji yeyote wa kompyuta. Mwezi Novemba 1993, ilipandishwa hewani na ndani ya mwezi mmoja tu tayari ilikuwa na watumiaji zaidi ya arobaini elfu (40,000). Miezi michache baadae kivinjari hiki kilikuwa na mamilioni ya watumiaji. Inaelezwa kuwa kivinjari cha Mosaic kiliweza kutatua matatizo makuu mawili:
Mosi, vivinjari kabla ya Mosaic vilikuwa havifanyi kazi vizuri. Pili, kivinjari hiki ndio kilikuwa cha kwanza kuweza kufanya tovuti yenye rangi/picha kuonekana vizuri bila shida yoyote.
Mwaka 1994, Bw. Marc Andreessen na timu yake waliondoka NCSA na kutengneneza toleo jipya la kivinjari hicho kwa lengo la kibiashara na kwa ukubwa zaidi na ndio hapo ilipotoka Netscape. Netscape ilikuja kuleta mapinduzi makubwa kwenye intaneti kutoka kuwa kifaa cha kufanyia tafiti tuu hadi kuwa maarufu kwelikweli.
Maboresho halikadhalika matumizi ya kivinjari cha Mosaic yalifikia tamati mwaka 1997. Wakati ule mtu hakuwa na pa kuchagua hiki sijakipenda ngoja nitumie hii tofauti na leo hii ambapo tuna vivinjari lukuki na vizuri tuu.
Vyanzo: IEEE ComSoc, NCSA
No Comment! Be the first one.