Majanga ya rununu kuingia kwenye maji ni vitu ambavyo watu wengi duniani kote wamepitia na kufanya simu zao kuharibika hivyo kuingia gharama kuzitengeneza.
Kila simu iko tofauti kulingana na uundaji wake/mfumo wa simu hivyo yakupasa uwe makini sana pale unapokausha maji kwenye simu yako. Fanya yafuatayo endapo simu yako ya aina hii imeingia maji.
- Simu zinazoingia maji haraka
Hizi ni simu ambazo hazina uwezo wa kuhimili uwepo wa maji.
- Utoe simu yako kwenye maji haraka, kuendelea kuiacha simu kwenye maji ndio kuendelea kuiharibu zaidi.
- Zima simu yako haraka sana unaweza kutumia kitufe cha kuzima simu au unaweza kutoa betri (kama simu yako inaruhusu).
Kumbuka simu yako inatumia umeme, kuendelea kuwaka ilihali kuna maji kwenye mkondo wa umeme ni mbaya zaidi unaweza kuunguza vifaa. Kwa maji ya chumvi, kilevi na vimiminika vingine tumia kitambaa chenye unyevunyevu, ndiyo kwa sababu chumvi japo utaweka maji kwenye simu tena lakini itasaidia kuondoa chumvi na pombe, simu nyingi zina shida na kitambaa chenye unyevu.
Toa vitu kama kadi ya simu, memori ya ziada na kama simu ina uwezo wa kutoa betri basi liondoe. Kipindi unatoa hivyo vitu kuwa makini sana usitingishe simu yako maana unaweza kuingiza maji kwenye mifumo ya simu. Baada ya hapo kausha simu yako kwa kutumia kitambaa kikavu, kuwa makini usiweke maji sehemu zenye uwazi kama mahali pa kuchomeka spika za nje, kuchaji, n.k, safisha sehemu ulizotoa kadi ya simu, memori ya ziada, na betri.
Usifanye yafuatayo:-
- Usiweke kitambaa wala chochote kwenye sehemu ya kuchajia.
- Usibonyeze kitufe chochote kwenye simu yako.
- Usitingishe wala usigeuze gauze simu yako.
- Usiweke karibu na feni (wengine mnajua hizi zinakausha maji lakini ni hatari).
- Usijaribu kuchaji simu yako.
- Usikaushe simu yako Kutumia vifaa kama mashine ya kukausha nywele.
Bada ya hapo
Weka simu yako juu ya Kitambaa chepesi kikavu au taulo laini kisha weka sehemu ambayo ni kavu ila siyo juani. Kisha subiri kwa siku moja au mbili bila kuigusa wala kuiwasha kwa kipindi cha angalau saa 48.
Vipi kuhusu kuweka kwenye mchele?
Wengi mnajua na mmeambiwa kuwa njia nzuri ya kukausha simu iliyoingia maji ni kuweka kwenye mchele ambao haujapikwa, ambapo mchele utafyonza unyevunyevu uliopo ndani ya simu ambao haukuweza kutoka pindi unakausha simu. Hii nadharia huenda ikafanya kazi au isifanye kazi kutokana na aina ya simu, simu nyingi za kisasa hazifunguliwi kwa maana ya kutoa betri na zina sehemu chache zenye uwazi hivyo inakuwa ngumu kwa mchele kufikia sehemu zenye maji au kufyonza maji kwenye simu.
2. Simu zisizoingia maji haraka
Hizi ni simu zinazoweza kuhimili uwepo wa maji kwa mda kadhaa, lakini haimaanishi haziwezi kupata madhara endapo zimeingia maji.
Cha kufanya endapo simu yako imeingia maji
- Zima simu yako haraka. Hapa bado kuna mkanganyiko, Baadhi ya waundaji wa smartphone wanasema “Hapana usizime” wengine wanasema “Ndiyo zima” Lakini kama una wasiwasi Basi unashauriwa kuzima simu, umenunua hela nyingi hiyo simu kwahiyo kinga ni bora zaidi.
- Kama ukiamua kuiacha simu yako inawaka basi usitumie vitu kama kama spika za nje za kuchomeka. Halikadhalika, Usichaji simu yako.
- Kwa maji ya chumvi, kileo na vimiminika vingine. Safisha simu yako kwa maji safi sababu chumvi hivyo inaweza kuharibu simu ya aina yoyote iwe haiingi maji. Vimiminika vingine pia vinaweza kuleta madhara hivyo ni muhimu kuisafisha simu kwa maji safi au kemikali yenye kilevi inayoitwa isopropyl, lakini simu haiwezi kuhimili maji yanayotiririka kwa kasi inakupasa uisafishie kwenye ndoo kwa mfano.
- Baada ya hapo ikaushe simu yako kwa kitambaa laini na kikavu. Usiweke kitambaa au chochote kwenye sehemu ya kuchomeka chaji. Usitoe kadi ya simu, memori ya ziada. Usikaushe simu yako kwa kutumia vitu kama mashine ya kukausha nywele.
No Comment! Be the first one.