Raisi wa Marekani Barrack Obama atajua nini kitamtokea John Snow mapema kabla ya mtu yeyote ( Ukiondoa waandaaji wa GOT), hii ni baada ya kuwaomba waandaji wa series hiyo kuona show hiyo kabla haijaanza kuoneshwa. Tamthilia hii huwa inazungumziwa sana mitandaoni.
Game Of Thrones ni tamthilia iliyojipatia umaarufu mkubwa kwa watazamaji wengi, moja ya mambo yaliyoipa tamthilia hii umaarufu ni mtindo wa watunzi wake kubadilisha hadithi kutoka katika hadithi halisi ambayo tamthiliya hiyo iliandikwa.
Mhusika John Snow katika tamthilia ya Game of Thrones
Katika toleo lililopita mmoja ya waigizaji wa tamthilia hii ambaye alikuwa anapendwa anayeitwa John Snow alionekana akiuwawa kitu ambacho kiliwahuzunisha wengi wanaoifuatilia tamthilia hiyo (mimi nikiwa mmoja wao) lakini tetesi zinasema kwamba John Snow ataonekana katika toleo lijalo na hii ndiyoimezidisha hamu ya kutaka kujua kilichomo katika toleo lijalo.
Waandaaji wa tamthilia hii wamekuwa ni wa siri wakubwa katika uandaaji wa tamthilia hii kitu ambacho kinapelekea watu wengi kutojua nini kitakuja kutokea katika toleo linalofata la GOT.
Miendelezo (episodes) za tamthilia hii zimekuwa zikiongoza katika kushushwa katika mitandao ya kimfumo wa Torrents duniani kote.
KAT
Hata hivyo waandaji hao wamesema kwamba raisi wa Marekani amewaomba kuona tamthilia hiyo mapema zaidi na wao wamemkubalia hivyo kumfanya mtu peke ambaye siyo muandaaji ambaye atajua mwisho wa John Snow kabla ya watu wengine wote.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.