Oppo ambao wanakuja kwa kasi kwenye suala zima la ushindani simu rununu ulimwenguni inatazamiwa kuishangaza dunia kwa toleo lijalo la simu janja inayofahamika kama Oppo Find X.
Sio mara moja tumeshawahi kuandika habari kuhusu bidhaa zinazotengenezwa na Oppo na kwa jinsi ambavyo zinapata soko zuri kuweza kushika nafasi za juu kushindana na makampuni nguli kama Apple na Samsung.
Kwa taarifa ambazo zipo zinaelezwa kuwa Oppo katika toleo lijalo la Find X huenda ikawa simu ya kwanza kuja na RAM ya GB 10.
Oppo Find X toleo la hivi sasa.
Oppo Find X ambayo ilizinduliwa mwezi Julai mwaka 2018 haitakuwa na utofauti mbali na ukubwa wa RAM na rangi ambapo kwa taarifa za awali zinasema Kahawia itakuwa miogoni mwa rangi ambazo itapatikana katika toleo lijalo.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|