Kampuni ya simu ya TECNO Mobile wamekuja na shindano linalohusisha simu yao mpya iliyoingia sokoni ya Tecno Boom J8. Katika shindano hilo lililopewa jina la #BoomJ8ParisTZ mshindi atapata nafasi ya kusafiri hadi jiji la Paris nchini Ufaransa.
‘Paris ni moja kati ya miji mashuhuri ulimwenguni kote ukiwa na vivutio mbali mbali. Ukiwa umeshikilia namba mbili ya miji inayovutia zaidi ulimwenguni umekuwa ukitembelewa na watu kutoka mataifa mbali mbali kila mwaka.
Kwa kupitia Boom J8 unaweza kushiriki katika shindano la #BoomJ8ParisTz kwa kushare wimbo unaupenda zaidi kutoka katika Boom Player kwenda katika ukurasa wako wa Facebook. Ukishafanya hivyo kilichobaki ni kuwataarifu washikaji waweze kulike.
Kushiriki ni rahisi na kushinda pia hakuhitaji kazi ngumu, kila siku mtu mmoja anajishindia Boom J8 mpyakwa kushare wimbo aupendao kutoka Boom Player, lakini pia kuna zawadi nyingine kibao.
Boom J8 imekuja na maajabu ambayo hutaacha kuipenda kila siku, kama unataka kwenda Paris itakapofika tarehe 23 Mei, Basi bonyeza http://goo.gl/qh78WU kushiriki katika shindano.’ – ilisomeka taarifa rasmi
Tupo njiani kuweka uchambuzi wa simu hii ya Tecno Boom J8 ndani ya wiki hii. Ingawa Tecno wanafamilia zingine za simu kama vile Phantom na Camon, simu za Boom zinawakilisha familia ya simu zinazowalenga wapenda muziki zaidi.
One Comment
Comments are closed.