Polisi Tanzania imekuwa ikifanya jitihada mbalimbali kuweza kukabiliana na wale ambao wanabainika kutumia vibaya mitandao ya kijamii.
Kundi hilo ambalo lina jukumu la usalama wa raia na mali zake imeweka wazi mpango wake wa kuwasaka viongozi wa makundi ya WhatsApp ambao wanaendesha mtandao huo kwa mambo yasiyofaa.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa inasema Polisi wanaendelea na uchunguzi wa kuwabaini wale wote wanaoendesha biashara ya kujiuza na kuweka picha za uchi kwenye mitandao ya kijamii hususani kwenye Whatsapp na Instagram.
Viongozi wa makundi ya kwenye WhatsApp watakiwa kujihadhari na mkono wa sheria kuwa sehemu salama.
WhatsApp, Instagram na intaneti kwa ujumla ni vitu ambavyo vinaweza kusaidia katika mambo mbalimbali na iwapo tukiitumia vyema daima tutaepkukana na fedhea za makosa ya mtandaoni.
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|