Siku ya jana (Julai 21) tuliandika kuhusu fununu za ujio wa Samsung Galaxy Fold 8 ambapo imezoeleka kuona bidhaa mpya kipindi hiki cha majira ya joto na hilo ni kweli kwani simu hiyo pamoja na nyinginezo za muundo huo zimezinduliwa!
Samsung imeendeleza desturi yake ya kutoa simu janja ambazo ni za kukunja na kukunjua lakini pia za hali ya juu katika mwezi Julai kila mwaka. Kwenye matangazo yaliyorushwa mukashara huko London leo hii saa 10 jioni muda wa Afrika Mashariki. Kwenye matangazo hayo Samsung pia wamezindua Galaxy Z Flip, Galaxy Z Fold 8 Ultra.
Galaxy Fold 8
Simu hii ndio ilikuwa habari kuu kwenye uzinduzi wa leo ikiwa imejaa sifa nzuri, za kuvutia na ukweli ni kwamba ni ghali, $1,900 | zaidi ya Tsh. 4,940,000 bei ya ughaibuni. Sifa kuu ni hizi:-
- Skrini (Display) Bora: Ina skrini ya AMOLED yenye uwezo wa
120Hz5.5-inchi ikiwa imekunjwa na 7.6 inchi kama imekunjuliwa. Hii inamaanisha kuwa picha na video zitaonekana kwa uwazi wa hali ya juu na utumiaji wake utakuwa laini sana. Ina kinga ya Flex Titanium inayohakikisha skrini inastahimili mikwaruzo na matone. - Betri Imara yenye Nguvu: Licha ya umbile lake jembamba, simu hii ina betri kubwa ya 4800mAh inayoweza kudumu siku nzima na kuchaji kwa waya 45W (0%-63% ndani ya dakika 30) na 20W bila kutumia chaji. Hii inakupa uhakika wa kutumia simu yako bila wasiwasi wa kuishiwa chaji.
- Kamera Zenye Ubora wa Juu: Mbali na muundo, simu hii ina mfumo wa kamera mbili 50MP nyuma na kamera mbili za mbele ya 10MP kwa ajili ya picha za selfie, ikiwa imekunjuliwa, 10MP kamera ya mbele ikiwa imekunjwa. Hii inahakikisha unapata picha na video zenye ubora wa 4K +kukuza picha mara 10. Uwezo wa kurekodi video za ubora wa 4K halikadhalika, uwezo wa kukuza picha mara 10.
- Utendaji wa Juu: Inatumia chipset ya Snapdragon 8 Elite Gen 5, teknolojia ya akili mnemba – Galaxy AI4
na mpaka 16GB ya RAM pamoja na hifadhi ya ndani ya hadi 1TB. Hii inakupa uwezo wa kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja na kuhifadhi faili zako zote muhimu. Ina uzito wa gramu 201.Samsung Galaxy Fold 8 ina teknolojia ya IP48 maana yake kutoingia maji kwa muda wa dakika 30 kwa umbali wa mita 1.5 chini ya maji. Pia, inatumia USB Type-C.
Galaxy Z Flip 8
Hii simu janja pia ina uwezo wa hali ya juu na inafanana kwa karibu kabisa na toleo la Galaxy Z Flip 7 iliyotoka mwaka 2025. Toleo jipya bei yake ya ughaibuni inaanzia $1,199 | zaidi ya Tsh. 3,117,400 bei ya ughaibuni. Mengineyo ni kama ifuatavyo:-
- Skrini (Display) Bora: Ina skrini ya Dynamic AMOLED yenye uwezo wa
120Hz4.1 inchi ikiwa imekunjwa na 6.9 inchi kama imekunjuliwa. Hii inamaanisha kuwa picha na video zitaonekana kwa uwazi wa hali ya juu na utumiaji wake utakuwa laini sana. Ina kinga ya Flex Titanium inayohakikisha skrini inastahimili mikwaruzo na matone. - Betri Imara yenye Nguvu: Licha ya umbile lake jembamba, simu hii ina betri kubwa ya 4300mAh inayoweza kudumu siku nzima na kuchaji kwa waya 45W (0%-63% ndani ya dakika 30) na 20W bila kutumia chaji. Hii inakupa uhakika wa kutumia simu yako bila wasiwasi wa kuishiwa chaji.
- Kamera Zenye Ubora wa Juu: Mbali na muundo, simu hii ina mfumo wa kamera mbili 50MP+12MP nyuma na kamera ya mbele ya 10MP kwa ajili ya picha za selfie. Hii inahakikisha unapata picha na video zenye ubora wa 8K+kukuza picha mara 10.
- Utendaji wa Juu: Inatumia chipset ya Snapdragon 8 Elite Gen 5, teknolojia ya akili mnemba – Galaxy AI4
na 12GB, 16GB ya RAM pamoja na hifadhi ya ndani ya 256GB | 512GB. Hii inakupa uwezo wa kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja na kuhifadhi faili zako zote muhimu.Galaxy Z Flip 8 ina teknolojia ya IP48 maana yake kutoingia maji kwa muda wa dakika 30 kwa umbali wa mita 1.5 chini ya maji. Pia, inatumia USB Type-C.
Galaxy Z Fold 8 Ultra
Simu janja hii ina mengi na bora zaidi kati ya zile ambazo zimezinduliwa kwa pamoja. Kuipata simu hii ni vyema ukajipanga vyema kwelikweli maana inauzwa kati ya $2,099~$2,699 | zaidi ya Tsh. 5,457,400 ~ Tsh. 7,017,400 bei ya ughaibuni. Sifa nyinginezo ni:-
- Skrini (Display) Bora: Ina skrini ya Dynamic AMOLED yenye uwezo wa
120Hz6.5 inchi ikiwa imekunjwa na 8.0 inchi kama imekunjuliwa. Hii inamaanisha kuwa picha na video zitaonekana kwa uwazi wa hali ya juu na utumiaji wake utakuwa laini sana. Ina kinga ya Flex Titanium inayohakikisha skrini inastahimili mikwaruzo na matone. - Betri Imara yenye Nguvu: Licha ya umbile lake jembamba, simu hii ina betri kubwa ya 5000mAh inayoweza kudumu siku nzima na kuchaji kwa waya 45W (0%-63% ndani ya dakika 30) na 20W bila kutumia chaji. Hii inakupa uhakika wa kutumia simu yako bila wasiwasi wa kuishiwa chaji.
- Kamera Zenye Ubora wa Juu: Mbali na muundo, simu hii ina mfumo wa kamera tatu 200MP+50MP+10MP nyuma na kamera ya mbele ya 10MP kwa ajili ya picha za selfie, ikiwa imekunjuliwa, 10MP kamera ya mbele ikiwa imekunjwa. Hii inahakikisha unapata picha na video zenye ubora wa 8K+kukuza picha mara 30.
- Utendaji wa Juu: Inatumia chipset ya Snapdragon 8 Elite Gen 5, teknolojia ya akili mnemba – Galaxy AI4
na 12GB | 16GB ya RAM pamoja na hifadhi ya ndani ya 256GB | 512GB | 1TB. Hii inakupa uwezo wa kufanya kazi nyingi kwa wakati mmoja na kuhifadhi faili zako zote muhimu.Galaxy Z Fold 8 Ultra ina teknolojia ya IP48 maana yake kutoingia maji kwa muda wa dakika 30 kwa umbali wa mita 1.5 chini ya maji. Pia, inatumia USB Type-C.
Simu hizi zote zinapatikana kwa kuagiza lakini zitaingia madukani Agosti, 7 2026 zikiwa na rangi mbalimbali kama kijivu, bluu. Una maoni gani kuhusu simu simu hizi? Tupe maoni yako.
Vyanzo: Samsung, CNET, Engadget, Mashable.
No Comment! Be the first one.