Facebook kwa sasa inaongoza katika mitandao ya kijamiii yenye huduma nyingi hii ni ukiachana na huduma zile za kawaida zilizo zoeleka kama kutuma na kupokea ujume na kupiga simu.
Facebook imezindua kipengele kingine rasmi kwa ajili ya waandishi wa habari (signal). Hii ikiwa msaada kwao juu ya kujikusanyia habari na matukio mbali mbali duniani
Kitu hiki kimefananishwa na kile cha twitter kinachoitwa ‘Trends’ ikiwa na maana ya ‘Mwenendo’. Unaweza ukadhani kipengele hiki ni cha Facebook peke yake lakini kinafanya kazi mpaka katika mtandao wa kijamii wa instragram unaohusisha picha na video.

Kipengele hiki kitasaidia waandishi wa habari kuvuna habari kupitia mitandao ya kijamii ya Facebook na instragam. Hebu fikiria ni matukio mangapi yanayotokea mtaani na raia wanakuwa wakwanza kuyaweka mtandaoni? jibu unalo! waandishi wa habari wanaweza tumia mitandao ya kijamii hiyo (facebook na instagram) ili kupata taarifa (habari) hizo
Signal pia ina vipengele vipya ambavyo havijawahi kutumika kama vile kile cha ‘Leaderboards’, ukurasa unaosaka na kuchambua data za mazungumzo katika maelfu ya kurasa, ambazo zinaweza kutumia kupima uhalisia wa yale yaliyoandikwa na majina makubwa kama vile wanamuziki na wanasiasa

Dashboard pia linatumika kumrusu mwandishi kuhifadhi picha na post zilizopatikana kutoka Facebook na Instagram na kuziweka katika sehemu ya mkusanyiko (Collections) ambapo baadae mwandishi anaweza aka ‘click’ mara moja ili kupata uwezo wa kupachika makusanyiko hayo yote katika sehemu (post) moja.
Hii ni njia mojawapo ya njia ya kuwasaidia waandishi wa habari ili kupata taarifa na matukio yenye ukweli juu yake. kama wewe ni muandishi wa habari na untaka kupata huduma hii kuna fomu ya kujaza hapa
No Comment! Be the first one.