Kwa sasa kuback up na kupakua mafaili uliyohifadhi ya whatsApp sio kitu kigumu. Sawa kila mtu anaweza akawa anaweza hili lakini vipi pale unapoibiwa, poteza au hata badilisha simu?
Inakua kazi ngumu, au sio?.Tatizo hili linawakuta mara nyingi watumiajj wa simu za Android.
Unaweza ukabadili simu yako lakini ukapata maudhi kidogo kwa sababu chati zako (za WhatsApp) ulizifanyia back up kwenye memori kadi ambayo umeuza ikiwa katika simu. Sasa unafanyaje?
Fununu zinasema kuwa WhatsApp wanaweza wakaanzisha mfumo mpya wa kufanya back up na hiyo itakua inafanyika na Google Drive. Hii itarahisisha kila kitu kwa sababu mtumiaji wa whatsapp anaweza fanya back up mda wowote na kwa urahisi tuu.
Watumiaji hawatafanya kazi kubwa kwa mikono yao bali kila kitu kitakua kikifanyika kirahisi tuu. Sio lazima mpaka waweke memori kadi zao. Hata hivyo kitu ukikihifadhi katika mtandao ndio kina nafasi kubwa ya kudumu kuliko kikiwa katika simu.
MUHIMU: Kwa sasa Back Up iliyochukuliwa katika simu ya Android itatumika tuu kwenye simu za Android, Pia itakua hivyo hivyo kwa simu za iOS, Windows na Blackberry.
Mabadiliko haya yatakua mazuri na yatapokewa sana na watumiaji wa Android, Windows na Blackberry. Watumiaji wa iOS kwa sasa wanafanya Back Up za chati zao za whatsApp katika iCloud. Kwa hiyo katika iPhone itakua ni chaguo la ziada na sio kitu kipya.
No Comment! Be the first one.