Kampuni ya Apple imetangaza rasmi kuwa Tim Cook atajiuzulu nafasi yake kama CEO / Mkurugenzi Mkuu ifikapo tarehe 1 Septemba 2026. Cook hatoki kabisa kwenye kampuni hiyo; badala yake, atahamia kwenye nafasi ya Mwenyekiti Mtendaji (Executive Chairman) wa bodi ya wakurugenzi ya Apple.

Nafasi yake itachukuliwa na John Ternus, ambaye kwa sasa ni Makamu wa Rais Mwandamizi wa Uhandisi wa Vifaa (Hardware Engineering). Ternus amekuwa na Apple kwa miaka 25 na anasifika kwa kusimamia ubunifu wa bidhaa kama iPad, iPhone, na hivi karibuni teknolojia ya Apple Silicon.
Chini ya uongozi wa Tim Cook tangu mwaka 2011, Apple imekua kutoka thamani ya dola bilioni $350 hadi kufikia zaidi ya dola trilioni $4, huku akianzisha bidhaa mpya kama Apple Watch, AirPods, na Apple Vision Pro.
Mambo 5 ya Kufahamu Kuhusu Tim Cook
Licha ya kuwa mmoja wa viongozi wenye nguvu zaidi duniani, Tim Cook anaishi maisha ya kipekee. Hapa kuna mambo matano usiyoyajua kumhusu:
- Mtu wa Mapema Sana: Cook anajulikana kwa kuamka saa 3:45 asubuhi kila siku. Anatumia saa ya kwanza kusoma barua pepe za wateja na wafanyakazi wake kabla ya kwenda kufanya mazoezi ya viungo (gym).
- Mtaalamu wa Uendeshaji /Operesheni: Tofauti na Steve Jobs aliyekuwa gwiji wa ubunifu wa bidhaa, sifa kuu ya Cook ni “Operations.” Kabla ya kuwa CEO, alikuwa mtaalamu wa kusimamia mnyororo wa usambazaji (supply chain), kitu kilichosaidia Apple kutengeneza faida kubwa kwa kupunguza gharama za uzalishaji.
- Alikubali kutoa Sehemu ya Ini Lake kwa Steve Jobs: Inasemekana mnamo mwaka 2009, Cook alijitolea kumpa Steve Jobs sehemu ya ini lake baada ya Jobs kuugua saratani. Jobs alikataa katakata akisema, “Sitakuacha ufanye hivyo.”
- Mpenzi wa Mazingira na Faragha: Chini ya uongozi wake, Apple imekuwa kampuni inayopigania sana faragha ya mtumiaji (privacy) na imepunguza uharibifu wa mazingira kwa zaidi ya 60% tangu mwaka 2015. Katika faragha ingawa Tim Cook alishakuwa wazi kuwa anashiriki mapenzi ya jinsia moja ila amejaribu sana kuficha maisha yake ya mahusiano.
- Mpango wa Kutoa Utajiri Wake: Cook amewahi kutangaza kuwa ana mpango wa kutoa karibu utajiri wake wote kwa kazi za kijamii na hisani (charity) kabla ya kufariki, akifuata nyayo za mabilionea wengine kama Bill Gates.
No Comment! Be the first one.