Ufaransa ni nchi kubwa sana na inajiweza katika mambo mengi kama vile kiuchumi. Ukiachana na kuwa taifa kubwa kuna mambo mengi ambayo raisi mpya wa nchi hiyo anataka kuyaboresha.
Baada ya mambo hayo ni ikiwemo na hili la kutaka mpaka kufikia mwaka 2040 kusiwe na magari yoyote ambayo yanatumia nishati ya petrol au diesel nchini ufaransa.

Na hili limetokea baada ya siku chache tuu kampuni ya Volvo kusema kuanzia mwaka 2019 itaanza kutoa magari yanayotuumia nishati ya umeme
Hili ni jambo zuri na linakuja kama njia moja ya kupunguza uharibifu wa mazingira (Hewa). Ni wazi kwamba mashine nyingi na ikiwemo magari huwa yanatoa hewa chafu ya ‘cabon’ ambayo inaharibu mazingira na inaathiri kwa kiasi kikubwa afya ya mwanadamu.

Kufikia lengo hili pia kwa watengenezaji wa magari wa ufaransa sio jambo la mchezo mchezo kwani makampuni hayo inabidi yaje na magari ambayo hayatatumia nishati hizo kabisa.
Makampuni kama Renault na Peugeot-Citroen ni makampuni makubwa sana duniani lakini yapo katika presha kutokana na jambo hili.
Vile vile Raisi wa ufaransa amesema kuwa mpaka kufikia 2022 matumizi ya makaa ya mawe hayatatakiwa tena na hivyo basi teknolojia hiyo itahimia na kutumia umeme.

Kingine kizuri ni kwamba wamekadiria kwamba kama magari yanayotumia nishati ya mafuta (petrol na diesel) yanakaa baeabarani kwa muda wa miaka kumi na tano. Hii ni sawa na kusema kuwa mpaka 2055 ufaransa kutakuwa hakuna magari ambayo yanatumia nishati hizo kabisa.
One Comment
Comments are closed.