Microsoft wameendelea kufikia tamati ya vitu vyao vya zamani na safari hii ni zamu ya programu endeshi nyingine kwa maana ya kwamba mmikiki ataacha kutoa ulinzi kwenye Windows 7.
Utakumbuka kuwa hii sio mara ya kwanza kwa wahusika kuamua kitu kama hicho kwani ilikuwa vivyo hivyo kwa Windows XP mwaka 2014. Masasisho yenyewe yanapatikana kwa baadhi ya walengwa tena kwa kulipia.
Kampuni/taasisi zinazotumia Windows 7 kwenye kompyuta zao watalipia ili kupata msaada wa kiusalama kwenye programu hiyo mpaka mwaka 2023 na baada ya muda huo mambo yatafikia mwisho kwa wote.
Ada za kupata masasisho hayo hazitakuwa zinafanana kuanzia mwaka 2020-23 bali zitakuwa zikipanda mwaka hadi mwaka mpaka hitimisho rasmi la kutoa masasisho litakapofikiwa.
Microsoft imeongeza muda wa mpaka miaka mitano kwa mashirika/taasisi kupokea masasisho kwenye Windows 7.
Ili kufanikiwa katika jambo fulani ni muhimu kutumia mbinu mbalimbali sasa Microsoft wametumia namna fulani ya kuongeza mauzo ya Windows tena; utalazimika kuboresha kutoka Windows 7 mpaka Windows 10 na mwisho wa siku idadi ya watumiaji itaongezeka.
Kama ulikuwa hufahamu fahamu sasa kwamba Windows 7 haina hata muongo mmoja tangu kuanza kutumiwa; ilizinduliwa mwaka 2009.
Vyanzo: Engadget, Tech Times
Timu ya uandishi wa Kona ya Teknolojia ingefurahi kupata sapoti yako ili iendelee kukuletea habari na maujanja mbalimbali.
Wezesha bando kwa kutuma kiasi chochote kupitia Selcom, kwenye simu yako bofya *150*50*1# kwenye namba ya malipo weka 60751369 jina litakuja TEKNOKONA.
Ni Mhariri Msaidizi na mtaalamu wa mambo yanayohusu kompyuta. Pia ni mmoja wa wafuasi wakubwa katika teknolojia; Dunia ya sasa inaendeshwa kwa teknolojia.
Wasiliana nami kupitia |ericmato@teknokona.com|