Wale ambao waliotaka kula iliwa bidi waende kwenye website ya kampuni au wapige simu ya kampuni hilo ili waletewe chakula. Sasa Google inakuja kutuokoa tena kwa
kutangaza kuwa sasa watu wataweza kuagiza chakula moja kwa moja kwa kutumia google search.
Ukiwa unatafuta migawa ya karibu (nearby restaurants) katika simu yako utaona chaguo la kuweka order (Place an order) katika majibu, Bofya hapo na chagua ungependa chakula chako kikufikie vipi.
Jinsi inavyofanya kazi ni kwamba mtumiaji wa simu anapoamua kutafuta mgahawa ambao unatoa huduma ya kutuma chakula kwa wateja wake katika Google, Google wataongeza chaguo la ‘Place an order’ ambapo mteja anaweza akaamua kupa click na kisha kuchagua jinsi anavyotaka chakula chake kumfikia kisha atafungiwa na kutumiwa
Kwa sababu ya hii kitu google inashirikiana na makampuni mengi ya kutoa huduma ya usafirishaji ili kukamilisha zoezi hili. Kwa sasa watumiaji wanaweza kuweka order zao katika migahawa ambayo inatumia huduma za usafirishaji kama vile Seamless, Grubhub, Delivery.com, Eat24, BeyondMenu, na MyPizza.com tuu.
Hata hivyo Google inasema inajitahidi kushirikiana na makampuni mengi haraka iwezekanavyo na sio hivyo tuu huduma hii inapatika sasa katika simu tuu. Na pia huduma hii inapatika US tuu kwa sasa lakini inaonekana kampuni itaongeza Inchi nyingine nyingi tuu.
Google imekua ikiongeza taratibu taratibu utendaji wa kazi wa ‘Search’. Google Now ina uewezo wa kumsaidia mtu kufanya vitu vingi sana ukiachana na ile progamu maarufu ya Apple, Siri hata na Cortana ya Microsoft. Wengi wanasema Google Now ndio msaidizi pekee wa mtu kwa sasa katika mtandao.
No Comment! Be the first one.