Je, ni vitu gani muhimu vya kuzingatia kabla ya kununua simu? Siku hizi simu ni za matumizi mengi sana zaidi ya kupiga na kupokea tuu, au kutuma ujumbe mfupi na kusoma tuu. Kuna mengi ya kutazama pale tunapotaka kununua simu inayoweza kuendana na mahitaji yetu.
Leo tutaangalia mambo kadhaa muhimu ya kuzingatia, kama kuna kitu tutakuwa tumekiacha ambacho ni muhimu sana kwako tafadhali tuambie kupitia kwenye comment hapa au kwenye akaunti zetu za mitandao ya kijamii. Hivi ndio vitu muhimu vya kuzingatia kabla ya kununua simu janja/rununu yako kwa sasa.
- Matumizi yako ya simu
Hatua ya kwanza kabisa ni kujitathimini na kutambua matumizi yako ya simu. Je huwa unatumiaje simu yako? Hili ni jambo la muhimu kwani aina ya matumizi yako ndiyo pia yanalenga bajeti unayotakiwa kuandaa kwa manunuzi ya simu husika.
Mfano:
- Kwa matumizi ya mawasiliano ya kawaida, kutumia WhatsApp na mitandao ya kijamii basi unaweza kupata simu nzuri tuu kwa bajeti isiyozidi Tsh. 500,000/=
- Kwa matumizi ya app nyingi, uchezaji magemu bila shida yeyote basi ni muhimu kuhakikisha wana bajeti ya kati ya Tsh 500,000 hadi Tsh. 900,000/=
- Kwa wale wanaopenda simu yenye uwezo kuhimili chochote, kuanzia magemu, masuala ya video na picha za ubora wa juu pamoja na simu zenye muonekano wa hadhi ya juu basi ni muhimu kuhakikisha bajeti ya Tsh. 900,000/= na zaidi iwe tayari. Kumbuka kuna simu za hadi Tsh 2,000,000/= na ushee siku hizi.
2. Programu Endeshaji: iOS au Android?
Je kuna simu ya Apple, yaani iPhone inauzwa kwa bei nafuu na unadhani itakuwa zuri zaidi kuliko kununua simu ya Android? Hapa kuna umuhimu sana wa kufahamu faida ya programu endeshaji moja dhidi ya nyingine. iOS ya kwenye iPhone ni nyepesi na haina mambo mengi, ila pia apps nyingi ni za kuuzwa na kuna vitu ambavyo kuvifanya vitahitaji uwe na kompyuta – hasa hasa kwenye usimamizi wa mafaili ya muziki, picha, n.k. Kwa Android kuna uhuru sana ila pia kama wewe ni mtu wa kudownload mafaili kutoka sehemu zisizoeleweka basi unaweza jikuta ukapata matatizo ya matangazo yasiyoeleweka kwenye simu yako, simu kuwa nzito n.k kwa urahisi.
Kwa mtu ambaye anapenda kudownload vitu mtandaoni, na asiye na kompyuta mara kwa mara, ushauri utakuwa ununue simu ya Android. Ila kwa wale ambao hawana matumizi ya namna hiyo, hawana mambo mengi kwenye simu zaidi ya mawasiliano ya kawaida na utumiaji wa apps za kawaida kama WhatsApp n.k basi wazo lako la kununua iPhone linaweza likawa bora zaidi.
3. Ujazo
Je, wewe ni mtu wa kupakua miziki mingi pamoja na filamu kwenye simu yako? Basi utahitaji simu ujazo mkubwa zaidi. Simu nyingi kwa sasa kwa wastani zinakuja na ujazo wa GB 32, 64, na 128 hapa ukiacha zile chache zinazoenda zaidi ya hapo. Kama ni mtu wa mafaili mengi basi unahitaji GB 64 na zaidi. Ila kama ni mtu wa kutumia simu kwa matumizi ya kawaida, apps zako chache, kupiga na kupokea simu basi simu ya GB32 au 64 itakufaa bila shida.
No Comment! Be the first one.