Shirika la kukabiliana na dawa za kusisimua misuli duniani WADA limewashtumu wadukuzi kutoka Urusi kwa kutoa faili za siri za matibabu za wanariadha wa Marekani walioshiriki katika michezo ya Olimpiki mjini Rio.
Wanariadha walioathirika ni pamoja na mchezaji wa tenisi Venus na Serena Williams pamoja na mchezaji wa mazoezi ya viungo Simone Biles.
Kundi linalojiita Fancy Bears lilikiri kufanya udukuzi huo kuhusu data ya WADA. Baada ya ufichuzi huo Bi. Biles alisema kuwa amekuwa akitumia dawa za kutuliza mtu kuhangaika.

Kundi hilo la udukuzi lilimshutumu kwa kutumia dawa ya kusisimua misuli lakini akasema kuwa amekuwa akifuata sheria ambapo udukuzi huo ulifanikiwa baada ya kundi hili kuingia kwenye database ambayo inatunza taarifa za kiafya za wanamichezo.

Shirika la wanamichezo wa viungo nchini Marekani lilisema kuwa mshindi huyo wa medali nne katika michezo ya Rio Olimpiki alipata ruhusa ya kutumia dawa hizo zilizopigwa marufuku na WADA.
Katika nyaraka hizo zilionyesha kuwa wana ndugu kutoka familia moja (Serena&Venus), Simone na mcheza mpira wa kikapu Elena Delle Donne wakupewa msamaha fulani katika upimaji wa afya uliojulikana kama ‘Therapeutic Use Exemptions‘ kwa miaka kadhaa ambao uliwawezesha kutumia madawa yaliyopigwa marufuku.
Hii si habari njema kwa wanamichezo hao ukizingatia na ubora waliokuwa nao michezoni na yawezekana kabisa nyaraka hizo zikawasabishia mabaya wahusika. Ingawa wadukuzi hao wameshtumiwa vikali lakini siku zote kitu kama ni cha ukweli hupingwa vikali.
Vyanzo: Telegraph, BBC