Katika kufanya nini? Ndiyo, kama kichwa cha habari kinavyosema, wakati huku kwetu bado wanafunzi wanaendeleza njia za kizamani na kubuni mpya za kuibia majibu au kufanya udanganyifu wakati wa mtihani, wanafunzi wa nchini China ndio wanaongoza katika matumizi ya teknolojia ya kisasa katika kufanya udanganyifu huo.
Kila kipindi cha mitihani walimu na hata baadhi ya shule zinatumia polisi katika kuhaha na kusaidia katika kugundua njia zitumiwazo na wanafunzi hao. Inasemakana ugumu wa mitihani yao pamoja na kuwa na mfumo unafanana wa nchi kama Tanzania wa kwamba mtihani wa mwisho kubeba miaka yote ya mtu aliyotumia shuleni unachangia katika kukuza tabia hii.

Kali zaidi imetokea hivi karibuni baada ya kugundulika ya kuwa vijana wameendelea zaidi kiteknolojia katika kuhakikisha wanafanikiwa katika kuibia kwa kutengeneza miwani ambayo inarekodi na kutuma picha hizo kwa mwingine. Hii ni katika mtihani maarufu zaidi ujulikanao kwa jina la Gaokao ambao unaweza kuufananisha na ule wa kuhitimu kidato cha sita kwa hapa bongo. Ukaguzi wa wanafunzi kuingia eneo la kufanya mitihani katika gaokao imebidi nao uwe wa kiteknolojia ya juu, na hivyo imekuwa kama vile mwanafunzi anapita uwanja wa ndege.

Hivi kijana wa kibongo akipata vifaa hivi si atafaulu mitihani yote hapa bongo, au wewe unaonaje?
One Comment