Je unafahamu nje ya huduma za huduma za kupiga simu na vifurushi vya intaneti kwa watumiaji wa kawaida Yas kupitia Yas Business ni mshirika muhimu katika sekta ya biashara na uchumi wa taifa kwa ujumla? Mwishoni mwa mwezi Mei, tukio la kishindo la Yas Business lilifanyika katika ukumbi wa Super Dome lilionesha sura tofauti kabisa ya kampuni hii — kama mshirika mkuu na wa kimkakati kwa biashara kubwa, za kati na ndogo nchini Tanzania.
Ushuhuda wa Kiuhalisia: Miaka ya Ushirikiano
Katika tukio hilo, mashirika kadhaa ya sekta binafsi yalitoa ushuhuda wa jinsi ushirikiano wao na Yas ulivyonyoosha na kurahisisha operesheni zao. Moja ya masimulizi yaliyovutia ni ya kampuni ya huduma ambayo ilianza kushirikiana na Yas tangu mwaka 2017, ikitumia miundombinu ya mawasiliano ya kampuni hiyo kuratibu na kusimamia wafanyakazi na mifumo yao (field operations) katika maeneo ya ndani ndani nje ya miji. Kwa kutumia huduma za Yas waliweza kurahisisha mawasiliano na kuboresha ufanisi wa shughuli zao bila wasiwasi wa kutopata huduma za mawasiliano.

Huduma Mpya za Kidijitali kwa Ajili ya Mapinduzi ya Viwanda
Kupitia Yas Business kuna masuluhisho mapya ya kiteknolojia yanayolenga kuongeza ufanisi wa makampuni:
SD-WAN: Mfumo wa kisasa wenye akili bandia wa kuunganisha ofisi nyingi za kampuni kwa usalama na gharama nafuu.
Private 5G Networks: Mitandao binafsi ya 5G maalum kwa ajili ya maeneo ya migodi na viwanda vikubwa ili kuendesha mitambo kwa njia ya mtandao.
IoT Solutions (Internet of Things): Masuluhisho yanayowezesha vifaa mbalimbali vya kibiashara kuwasiliana vyenyewe kwa vyenyewe bila muingiliano wa kibinadamu.
Mchango kwenye Miradi ya Kitaifa
Mbali na biashara binafsi, Yas ilionesha mchango wake mkubwa katika maendeleo ya nchi. Kampuni imechangia asilimia 33 ya minara 758 iliyokabidhiwa kwa serikali hivi karibuni, pamoja na kutandaza zaidi ya kilomita 1,100 za nyaya za mawasiliano ya kasi ya juu ya fiber optic. Huduma inayowafikia watumiaji wa majumbani na wale wa biashara.
Kwa mwelekeo huu, Tanzania inazidi kupiga hatua kuwa kitovu kikuu cha dijitali (digital hub) kwa nchi za Afrika Mashariki. Kupitia Yas Business kwa biashara yoyote ile leo, swali sio tena “Je, tunahitaji teknolojia?” bali ni “Ni mshirika gani wa teknolojia mwenye viwango anayefaa kubeba maono yetu ya kibiashara?”
#YasBusiness #TeknolojiaBiashara #TanzaniaDigital #KonayaTeknolojia

No Comment! Be the first one.